Sunday, March 2, 2025

Home
Unlabelled
MIXX BY YAS YAWAFIKIA WAKAZI WA MTWARA YATOA ZAWADI YA MILIONI 20 KWA MSHINDI WA MAGIFTI YA KUGFTI
MIXX BY YAS YAWAFIKIA WAKAZI WA MTWARA YATOA ZAWADI YA MILIONI 20 KWA MSHINDI WA MAGIFTI YA KUGFTI
Hatimaye kampeni ya Magift inayofanywa na kampuni ya Yas Tanzania ,kupitia kitengo cha Mixx by Yas imeweza kuwazawadia, wateja na washindi wake wa mkoa wa mtwara zawadi mbalimbali, ikiwemo fedha na gari Moja.
Akizungumza mara baada ya kuibuka mshindi wa kampeni ya Mixx by Yas, Zena Ponera ambaye ni mkazi wa manispaa ya Mikindani mjini mtwara ameelezea MIKINDANI Siri ya ushindi huo, ambapo mbali na mambo mengine amesishukuru Yas kwa kufanikisha kuchezesha Droo za Magift ya KUGIFT 2024-25.
Kwa upande wake Meneja wa Yas Kanda ya Mtwara, Eric Munuku,ameelezea namna kampeni hiyo ilivyoweza kuwanufaisha watanzania wengi ambao wameweza kujishindia zawadi mbalimbali zikiwemo fedha magari na zawadi za simu za mkononi Kutoka Yas na Mixx by Yas.
Kampuni ya mtandao wa Mawasiliano ya Yas Tanzania kwa kipindi cha miezi miwili na nusu iliyopita iliendesha kampeni hiyo nchi ambapo jumla ya washindi Zaidi 300 walifanikiwa kujinyakulia zawadi mbalimbali Kutoka Kampuni ya Yas Tanzania.
Share This
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
SIMTANK TANZANIA YATOA ZAWADI KWA MAWAKALA WAKE WAKISHEREHEKEA MIAKA 35 TANGU KUANZISHA
Mwanzilishi wa Kampuni ya Silafrika Tanzania inayozalisha bidhaa za Simtank, Gulab Shah (wapili kushoto), akikabidhi cheti na zawadi ya ...
No comments:
Post a Comment