Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Waajiri wafanyika Dar. - Serious Business

Mgongopr.blogspot.com is a serious online platform of business and finance news from around Tanzania. We are a trusted site covering the entire spectrum, from small enterprises to large businesses entities. For photography, videography, media management, events management, advertising, public relations, translation, interpreters, and more services, please contact us: MPP Ltd phone: +255 767765454, email: mgongo@gmail.com

Breaking

Friday, June 30, 2017

Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Waajiri wafanyika Dar.

Waziri wa Viwanda  Biashara na Uwekezaji,  Mh Charles Mwijage (kushoto), akizungumza na aliyekuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Chama cha Waajiri Tanzania (ATE) Mh. Almas Maige (kulia), huku Mkurugenzi Mtendaji wa ATE, Dk. Aggrey Mlimuka akisikiliza wakati wa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa chama hicho jijini Dar es Salaam jana.

Waziri wa Viwanda  Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage (wa pili kushoto) akilakiwa na aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), Almas Maige (kushoto), na Mratibu wa Mradi wa Mwanamke wa Wakati Ujao,  Lilian Machera (kulia) alipokuwa mgeni rasmi katika Mkutano Mkuu wa Mwaka wa chama hicho, Dar es Salaam jana.
Mwenyekiti Mpya wa Bodi ya  Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), Mama Jayne Nyimbo (wa pili kushoto), akizungumza mara baada ya kuchaguliwa kushika nafasi hiyo wakati wa Mkutano Mkuuu wa Mwaka wa chama hicho jijini Dar es Salaam jana. Wengine kutoka kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa ATE, Dk. Aggrey Mlimuka, aliyekuwa mwenyekiti wa chama hicho, Mhe. Almas Maige na Makamu Mwenyekiti mpya, Felix Kagisa
Mkurugenzi  Mtendaji wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), Dk. Aggrey Mlimuka (kushoto), akiwa na baadhi ya maofisa wa chama hicho wakati zoezi la kuhesabu kura likiendelea.
Baadhi ya washiriki wa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), wakisikiliza hotuba mbalimbali zilizokuwa zikitolewa.

Baadhi ya washiriki katika mkutano huo wakimsikiliza Waziri wa Viwanda, Charles Mwijage ambaye alisema serikali itaendela kujenga mazingira mazuri ya utoaji vibali vya uwekezaji ili kuweza kufikia ajenda yake ya kuimarisha uchumi wa viwanda
Aliyekuwa Mwenyekiti Bodi ya  Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), Mhe. Almas Maige akizungumza wakati wa mkutano huo uliofanyika pamoja na mkutano kujadili masuala mbali mbali kuhusu ajira na uwekezaji. (All photos by Mgongos Photography)

No comments:

Post a Comment

Airtel Tanzania Yawapa Walimu Mafunzo ya Ujuzi wa Kidijitali Kupitia Mpango wa SmartWASOMI

Mkurugenzi wa Machapisho na Utafiti kutoka Taasisi ya Elimu Tanzania (TET), Bw. Kwangu Zabron Masalu (Katikati), akizungumza jijini Dar es S...

Pages