Serikali yaupongeza Mfuko wa PEPFAR ukitimiza miaka 20 ya kurudisha matumaini ya wenye VVU nchini - Serious Business

Mgongopr.blogspot.com is a serious online platform of business and finance news from around Tanzania. We are a trusted site covering the entire spectrum, from small enterprises to large businesses entities. For photography, videography, media management, events management, advertising, public relations, translation, interpreters, and more services, please contact us: MPP Ltd phone: +255 767765454, email: mgongo@gmail.com

Breaking

Wednesday, November 15, 2023

Serikali yaupongeza Mfuko wa PEPFAR ukitimiza miaka 20 ya kurudisha matumaini ya wenye VVU nchini

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Bi. Halima Dendego, akipokea cheti cha shukurani kwa kutambua mchango wake katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Ukimwi na unyanyapaa kwa wenye VVU katika Mkoa wa Iringa, kutoka kwa Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Marekani la maendeleo ya Kimataifa (USAID), Bwana Craig Hart, wakati wa ziara ya waandishi wa habari mkoani humo leo ikiwa ni sehemu ya matukio kuadhimisha miaka 20 ya Mfuko wa Dharura wa Rais wa Marekani wa kukabiliana na Ukimwi (PEPFAR). Ziara hiyo, ililenga kuangalia mafanikio ya miradi inayohudumia wenye VVU na kusimamiwa na mashirika ya Deloitte, Nacopha na FHI360.
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Marekani la maendeleo ya Kimataifa (USAID), Bwana Craig Hart, akikabidhi cheti cha shukurani kwa Mkurugenzi wa mradi wa USAID Afya Yangu Kanda ya Kusini Dk. Marina Njelekela, kwa kutambua mchango wa shirika hilo, likiwa ni moja ya Mashirika yanayofadhiliwa na Shirika la USAID katika kutoa huduma bora kwa wenye VVU. Hii ni sehemu ya matukio ya kuadhimisha miaka 20 ya mfuko wa PEPFAR Mkoani Iringa leo. Wa kwanza kushoto ni muwakilishi wa PEPFAR nchini, Bi. Jessica Greene na Mkurugenzi Msaidizi wa USAID kitengo cha afya nchini, Bi. Anna Hofmann.
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID), Bwana Craig Hart, akikabidhi cheti cha shukurani kwa Mkurugenzi wa Mradi wa USAID Kizazi Hodari Kanda ya Kusini, Bi. Dorothy Matoyo (kulia) kwa kutambua mchango wa shirika hilo, likiwa ni moja ya Mashirika yanayofadhiliwa na Shirika la USAID katika kutoa huduma bora kwa wenye VVU. Hii ni sehemu ya matukio ya kuadhimisha miaka 20 ya mfuko wa PEPFAR Mkoani Iringa leo. Wa kwanza kushoto ni mwakilishi wa PEPFAR nchini, Bi. Jessica Greene na Mkurugenzi Msaidizi USAID kitengo cha afya nchini, Bi. Anna Hofmann.
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Marekani la maendeleo ya Kimataifa USAID Craig Hart, akikabidhi cheti cha shukurani kwa Mkurugenzi wa mradi wa Rise project, Maende Makokha, kwa kutambua mchango wa shirika hilo, likiwa ni moja ya Mashirika yanayofadhiliwa na Shirika la USAID katika kutoa huduma bora kwa wenye VVU. Hii ni sehemu ya matukio ya kuadhimisha miaka 20 ya mfuko wa PEPFAR Mkoani Iringa leo. Kushoto ni mwakilishi wa PEPFAR nchini, Jessica Greene na Mkurugenzi Msaidizi USAID Kitengo cha Afya nchini, Bi. Anna Hofmann.
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Marekani la maendeleo ya Kimataifa (USAID), Bwana. Craig Hart, akikabidhi cheti cha shukurani kwa Mkurugenzi wa Shirika la FHI360, Bwana Bernard Ogwang, kwa kutambua mchango wa shirika hilo, likiwa ni moja ya Mashirika yanayofadhiliwa na Shirika la USAID katika kutoa huduma bora kwa wenye VVU. Hii ni sehemu ya matukio ya kuadhimisha miaka 20 ya mfuko wa PEPFAR Mkoani Iringa leo
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID), Bwana Craig Hart, akikabidhi cheti cha shukurani kwa Mkurugenzi wa Shirika wa Nacopha, Bwana Deogratius Rutatwa, kwa kutambua mchango wa shirika hilo, likiwa ni moja ya Mashirika yanayofadhiliwa na Shirika la USAID katika kutoa huduma bora kwa wenye VVU. Hii ni sehemu ya matukio ya kuadhimisha miaka 20 ya mfuko wa PEPFAR Mkoani Iringa.
Mratibu wa Mfuko wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Kukabiliana na Ukimwi (PEPFAR) nchini, Bi. Jessica Greene akizungumza katika hafla hiyo.
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID), Bw Craig Hart (katikati), akipozi kwa picha ya kumbukumbu mjini Iringa leo, na baadhi ya wawakilishi kutoka mfuko wa PEPFAR, USAID na Mashirika yanayoratibu miradi ya Ukimwi inayofadhiliwa na PEPFAR kwa usimamizi wa USAID.

*Zaidi ya Dola za Kimarekani Bilioni 6 zatumika

*Mwaka 2022 pekee ikitumia Dola 450 milioni kupambana na maambukizi ya ukimwi nchini

Na Zuhura Rashidi, Iringa

SERIKALI ya Tanzania imeupongeza Mfuko wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Kukabiliana na Ukimwi (PEPFAR), kwa jitihada zake katika kuleta matumaini mapya katika mikoa iliyoelemewa na mzigo mkubwa wa maambukizi ya ugonjwa wa HIV na Kifua Kikuu.

Pongezi hizo zimetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Bi. Halima Dendegu wakati wa ziara ya wawakilishi wa mfuko wa PEPFAR, Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID), mashirika yanayotekeleza miradi ya ukimwi pamoja na waandishi wa habari mkoani humo wakitembelea miradi na vituo vinavyotoa huduma za ukimwi ikiwa ni sehemu ya matukio kuadhimisha miaka 20 tokea kuanzishwa kwa mfuko huo.

Mkuu wa Mkoa huyo alisema Iringa ni mmoja wa mikoa iliyoathiriwa sana na maambuki ya VVU lakini kwa msaada wa PEPFAR chini ya Shirika la USAID imewawezesha kuwa na vituo vya huduma na tiba (CTC) 261 kutoka vinane vilivyokuwepo awali, huku 136 vikiendeshwa na USAID vilivyosaidia kuleta mabadiliko chanya katika utoaji elimu na huduma bora kwa kutumia vifaa vilivyoboreshwa na wahudumu wa afya wenye elimu na ujuzi katika utoaji wa huduma bora za afya.

Tafadhali pokeeni pongezi za dhati kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassani, tunashukuru sana kwa misaada tunayoipokea kwani tunatarajia kushuka kwa maambukizi mapya kwa magonjwa ya ukimwi, kifua kikuu huku tukiendelea kupunguza unyanyapaa kwa wenye VVU."

Awali akizungumza mafanikio miradi ya PEPFAR inayosimamiwa na USAID, Mkurugenzi Mkazi wa shirika hilo nchini, Bwana Craig Hart alisema tokea mwaka 2003 serikali ya Marekali imetoa zaidi ya Dola za Kimarekani Bilioni 6 ikiwa ni pamoja na Dola 450 Milioni kwa mwaka 2022 pekee katika kupambana na ugonjwa wa Ukimwi chini Tanzania.

Mwaka 2003 ni watanzania 1000 tu waliokuwa wakipokea dawa za kupunguza makali ya VVU (ARV), leo wakati tukiadhimisha miaka 20 ya PEPFAR zaidi ya watanzania milioni 1.5 wananufaika na mpango huu wa tiba wa kuokoa maisha yao ikiwa ni asilimia 98 ya watu wanaoishi ya VVU."

Misaada yetu kwa watu wa Tanzania ni uwekezaji wa baadae, kwani kufikia mwaka 2050 robo ya watu wote duniani wataishi Afrika, nchini Tanzania theluthi mbili ya idadi ya watu wakiwa ni vijana chini ya umri wa miaka 25, hivyo kufanya uwekezaji katika kizazi kijacho kuwa ni jambo muhimu mno na lisiloepukika”, anasema Bwana Hart.

Naye Mratibu wa Mfuko wa PEPFAR nchini Bi. Jessica Greene alimpongeza Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa kugusia maeneo manne ambayo mfuko huo umekuwa ukiyapa kipaumbele akiyataja kama; tiba, utoaji huduma bora, vituo vya afya na dawa za kupunguza makali ya VVU.

Tumeungana na Serikali ya Tanzania katika kuhakikisha vipaumbele hivi vinafanikiwa na tutandelea kuhakikisha watu wenye VVU wanapata huduma boza za matunzo na tiba”, alisema Bi. Jessica.

Baadhi ya miradi inayofadhiliwa na PEPFAR chini ya usimamizi wa USAID ni USAID Afya Yangu Kanda ya Kusini unaolenga utoaji huduma jumuishi za matunzo, matibabu na kuzuia maambukizi ya VVU na kifua kikuu na kuboresha mazingira wezeshi ya utoaji wa huduma bora za afya katika mikoa sita ya kusini mwa Tanzania, huku mradi wa USAID Kizazi Hodari Kusini unaoangalia utoaji wa huduma jumuishi za watoto yatima na wanaoishi katika mazingira hatarishi pamoja na walezi wao ili kuboresha afya, ustawi na ulinzi wa watoto yatima pamoja na vijana katika mikoa 11, miradi hii ikiendesha na Shirika la Deloitte.

Mradi mwingine ni ‘Epic’ unaotekelezwa na Shirika la FHI360 uKjjikita katika kufikia na kuendeleza udhibiti wa janga la VVU huku ukijihusisha katika kutoa msaada wa kitaalamu na huduma za moja kwa moja katika kuondoa vikwazo kufikia malengo ya 95-95-95 ukilenga makundi maalumu wakiwemo wasichana, wamama vijana, wanaume na wanawake walio katika hatari ya kupata maambukizi ya VVU.

Aidha mradi wa ‘Hebu Tuyajenge’ ukishirikisha watu wanaoishi na VVU, unalenga katika kuongeza matumizi ya huduma za upimaji VVU, tiba na uzazi wa mpango mongoni mwa vijana balehe na wenye VVU ukitekelezwa na Baraza la Taifa la Watu wanaoishi na VVU Tanzania (NACOPHA).

No comments:

Post a Comment

Absa Dar City Marathon 2024 zatimua vumbi jijini Dar es Salaam

Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Absa Tanzania, Bwana Aron Luhanga (kushoto), akikabidhi zawadi kwa mshindi wa kwanza wa mbio za nu...

Pages