BARAZA LA MADIWANI ILALA LAPITISHA BAJETI YA BILION 287 - Serious Business

Mgongopr.blogspot.com is a serious online platform of business and finance news from around Tanzania. We are a trusted site covering the entire spectrum, from small enterprises to large businesses entities. For photography, videography, media management, events management, advertising, public relations, translation, interpreters, and more services, please contact us: MPP Ltd phone: +255 767765454, email: mgongo@gmail.com

Breaking

Monday, March 5, 2018

BARAZA LA MADIWANI ILALA LAPITISHA BAJETI YA BILION 287

Mwanasheria wa Manispaa ya Ilala Bonaventure Mwambaja akifafanua jambo wakati wa mkutano wa Baraza la Madiwani wa Manispaa hiyo leo jijini Dar es Salaam ambapo baraza hilo limepitisha bajeti ya sh.bilioni 287 kwaajili ya maendeleo ya wananchi katika mwaka wa fedha wa 2018/2019  ikilinganishwa na bajeti iliyopita ya 2017,2018 ya sh.bilioni 124.
Diwani wa Segerea Edwin Mwakatobe akichangia hoja wakati wa mkutano wa Baraza la Madiwani wa Manispaa hiyo leo jijini Dar es Salaam ambapo baraza hilo limepitisha bajeti ya sh.bilioni 287 kwaajili ya maendeleo ya wananchi katika mwaka wa fedha wa 2018/2019  ikilinganishwa na bajeti iliyopita ya 2017,2018 ya sh.bilioni 124
Mchumi wa Manispaa ya Ilala, Ando Mwanduga akizungumza na waandishi wa habari pamoja na jopo la madiwani wakati wa mkutano wa Baraza la Madiwani wa Manispaa hiyo leo jijini Dar es Salaam ambapo baraza hilo limepitisha bajeti ya sh.bilioni 287 kwaajili ya maendeleo ya wananchi katika mwaka wa fedha wa 2018/2019  ikilinganishwa na bajeti iliyopita ya 2017,2018 ya sh.bilioni 124. (Kushoto) ni Mwenye wa Baraza hilo ambae ni Mstahiki Meya Manispaa ya Ilala, Mhe Charles Kuyeko (kulia) Katibu Tawala ilala Edward Mpogolo 


Baraza  la Madiwani Manispaa ya Ilala limepitisha bajeti ya sh.bilioni 287 katika mwaka wa fedha wa 2018/2019  ikilinganishwa bajeti iliyopita ya 2017,2018 ya sh.bilioni 124.

Akizungumza na waandishi habari jijini Dar es Salaam, Mchumi wa Manispaa hiyo, Ando Mwanduga amesema kuwa bajeti hiyo katika sehemu kubwa ni kwa ajili ya maendeleo ya wananchi ambapo itahudumia kila mmoja bila ubaguzi.

Amesema kuwa  fedha hizo zitapatikana katika makundi mawili ya ruzuku pamoja na vyanzo vya mapato ya ndani ambapo hakuna mwananchi atakayeonewa katika bajeti hiyo.


Amesema kuwa chanzo cha mapato ya ndani  wanatarajia kukusanya sh.bilioni 56.8 ambapo  na fedha nyingine zitakuwa ni za ruzuku.

"Hakuna mwananchi atakayeonewa kwani tunakusanya kodi kikamilifu na katika chanzo CGA mapato yetu ya ndani tunatarajia kukusanya sh.bilioni 56.8 na fedha nyingine zitakuwa ni ruzuku" Amesema Mwanduga.

Mwanduga amesema kuwa kila diwani anataka kuwa na mradi katika kata yake lakini haiwezikani kutokana na uwezo wa manispaa hivyo wameweka mikakati katika kuahakikishawanakuza uchumi kutokana na mapato ya ndani .


Ameongeza kuwa bajeti hiyo itakayotekelezeka ni pamoja  na vyanzo hivyo viwili vya ruzuku na mapato ya ndani na asilimia 60 ni kwa ajili ya maendeleo ya wananchi katika kutekeleza miradi mbalimbali katika kata.

Aidha amesema kuwa kutokana na serikali ya awamu ya tano ya elimu bure kwa manispaa imethubu ikiwa ni pamoja na kujenga shule nne pamoja na kufanya ukarabati wa madarasa pamoja na majengo kwa bajeti hiyo.

No comments:

Post a Comment

Airtel, UNICEF wakabidhi Vifaa vya Intaneti ya kasi kwa Shule 30 za Sekondari Dodoma

Mwakilishi wa Afisa Elimu Sekondari Mkoa wa Dodoma, Bi. Grace Samweli, (Kulia) akipokea moja ya vifaa vya intaneti kutoka kwa Meneja wa Kand...

Pages