Thursday, March 29, 2018

RC MAKONDA AFANYA JAMBO HILI KWA WAMAMA WAJAWAZITO.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Dk. Grace Maghembe, (kushoto), akikabidhi vifaa tiba vya Mama mzazi kwaajili ya kujifungulia (Delivery Packs) kwa Mganga Mkuu wa Meno, wilaya ya Ubungo Safaa Chunga, kwa niaba ya Mganga Mkuu wa wilaya hiyo, hafla yamakabidhiano hayo imefanyika katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Dk. Grace Maghembe, akizungumza na waandishi wa habari kabla yakukabidhi vifaa hivyo
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda leo ametoa zawadi ya vifaa tiba vya Mama mzazi kwaajili ya kujifungulia (Delivery Packs) 200 vyenye thamani ya zaidi ya shilingi million 20 Kama zawadi yake ya sikukuu ya pasaka kwa kinamama watakaojifungua kwenye msimu huu wa pasaka.
Gharama ya mfuko mmoja (package) ya Vifaa hivyo vya kisasa ni Shilingi laki Moja ambapo ndani yake kuna Mashuka, Vitambaa, Dawa, Mabomba ya Sindano, Pamba, Kibanio cha kitovu, Nyuzi, pedi za kinamama, Dawa ya kuzuia upotevu wa damu, Nyembe na Gloves ambapo vitatolewa Bure kwa Mama mzazi atakaejifungua msimu huu wa pasaka kwenye vituo vya Afya na zahanati zilizopo kwenye Wilaya Tano za Mkoa huo.
RC Makonda ametoa vifaa hivyo baada ya kubaini changamoto ya baadhi ya kinamama kushindwa kumudu gharama ya vifaa vya kujifungulia na kujikuta wanatumia kanga au nguo jambo ambalo ni hatari kiafya kwa mama na mtoto.
Akikabidhi vifaa hivyo kwa niaba ya RC Makonda kwa waganga wakuu wa halmashauri na wasimamizi wa vituo na Zahanati, Mganga mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Dr. Grace Maghembe amesema vifaa hivyo vitasaidia pia kupunguza vifo vya mama na mtoto wakati wa kujifungua.
Vifaa hivi vinapatikana Bure kwenye Hospitali zote za Mkoa wa Dar es Salaam kwa Msimu huu wa Pasaka hivyo kwa wewe Mama unaetaka kujifungua fika Hospitalini vifaa vyako utavikuta.
KUTOA NI MOYO, SIO UTAJIRI.
Tags
# KITAIFA
Share This
Newer Article
Washindi wa Kampeni ya Akaunti ya Malengo ya NBC wa Mbeya na Mwanza waondoka na ‘Kirikuu’ zao
Older Article
Zantel yazindua progam maalumu kusaidia wahitimu wa vyuo kupata ajira moja kwa moja Zantel
MHE.HEMED ABDULLA AFUNGUA KITUO CHA AFYA CHA UZI NA NG'AMBWA
Hassani MakeroDec 27, 2023Shirika la USAID laipongeza serikali ya Tanzania mafanikio katika miradi ya elimu na afya nchini
Hassani MakeroNov 17, 2023Takwimu sahihi nyenzo muhimu mapambano dhidi ya Ukimwi
Hassani MakeroNov 16, 2023
Labels:
KITAIFA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Dk. Grace Maghembe, (kushoto), akikabidhi vifaa tiba vya Mama mzazi kwaajili ya kujifungulia (Delivery Packs) kwa Mganga Mkuu wa Meno, wilaya ya Ubungo Safaa Chunga, kwa niaba ya Mganga Mkuu wa wilaya hiyo,...
No comments:
Post a Comment