RC MAKONDA AITAKA DAWASCO KUONGEZA JITIHADA KATIKA KUSAMBAZA MAJI - THINKING IN BUSINESS

Mgongopr.blogspot.com is a business centered online platform highlighting trade, finance and economic news in Tanzania. Our coverage is customised to ensure we consolidate brands, boost sales and nurture investments. The site is an imprint of Mgongo Logistics and Solutions, a trusted consultancy firm, offering Social Media Management, Photography, Videography, Advertising, Event Management and Translation. For more information contact us via; Phone: +255 767765454, email: mgongo@gmail.com

Breaking

Saturday, March 17, 2018

RC MAKONDA AITAKA DAWASCO KUONGEZA JITIHADA KATIKA KUSAMBAZA MAJI




Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam  Mhe. Paul Makonda  amelitaka Shirika la Maji Safi na Maji Taka  DAWASCO kuhakikisha linashughulikia  kero zote za maji  kwa Wananchi ikiwemo kuhakikisha upatikanaji wa maji safi na kupatia ufumbuzi  tatizo la Maji Taka  yanayotiririka holela kwenye  makazi ya watu.


 Makonda ametoa agizo hilo wakati wa uzinduzi wa  Wiki ya Maji  ambapo amesema tatizo la  maji taka  limekuwa   kero sugu  katika maeneo mbalimbali ya jiji hilo  jambo linalohatarisha hata Afya za wananchi.


Aidha  Mhe,  Makonda  ameitaka  DAWASCO  kuongeza jitihada za kufikisha huduma ya maji kwa wananchi ili kuenda sambamba na  sera ya Serikali ya awamu ya Tano ya kumtua mama ndoo kichwani.

Hata hivyo  Makonda  ametoa wito kwa watumishi wa  DAWASCO wanaokwenda kusoma mita  kwa wananchi kuwa na lugha nzuri  kwa wananchi pamoja na kushughulikia  kero ya wananchi kubambikiziwa kiwango kikubwa cha malipo ya bili za maji.

Kuhusu changamoto ya  upotevu wa maji Mhe, Makonda  amelitaka shirika hilo kulipatia majibu ya haraka tatizo hilo ili kiasi cha maji yanayopotea kiweze kuwahudumia wananchi.

Ili kufikisha huduma ya maji kwa  maeneo yenye changamoto RC Makonda  amejitolea kuchimba  visima 50  vya maji ambapo amewasihi Wenyeviti wa mitaa hiyo kuainisha maeneo ya  kuchimba visima hivyo.

Pamoja na hayo Makonda  ametaka uwepo wa  ushirikiano wa kikazi baina ya TANROAD, TANESCO, TARURA na DAWASCO  ili kumaliza changamoto ya kukatwa kwa miundombinu ya maji  wakati wa ujenzi wa barabara pamoja na  uharibifu wa barabar

No comments:

Post a Comment

ABSA BANK TANZANIA SEES GLOBAL VOLATILITY AS A CATALYST FOR TANZANIAN COMPETITIVE ADVANTAGE

Corporate Banking Director at Absa Bank Tanzania, Ms. Nellyana Mmanyi, addresses participants during a meeting organized for senior business...

Pages