NBC kusaidia wanafunzi wanaoshindwa kumudu gharama za ada chuo kikuu - Serious Business

Mgongopr.blogspot.com is a serious online platform of business and finance news from around Tanzania. We are a trusted site covering the entire spectrum, from small enterprises to large businesses entities. For photography, videography, media management, events management, advertising, public relations, translation, interpreters, and more services, please contact us: MPP Ltd phone: +255 767765454, email: mgongo@gmail.com

Breaking

Sunday, December 1, 2019

NBC kusaidia wanafunzi wanaoshindwa kumudu gharama za ada chuo kikuu


Meneja Chapa na Mawasiliano wa NBC, David Raymond (kulia), akizungumza na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika hafla ya kuchangisha fedha kwa njia ya vichekesho na burudani iitwayo ‘Cheka Nisome’ iliyodhaminiwa na NBC yenye lengo la kuwasaidia wanafunzi wanaoshindwa kuendelea na masomo kutokana na kushindwa kumudu gharama za ada. Hafla hiyo ilifanyika chuoni hapo jijini Dar es Salaam juzi. Hafla hii iliratibiwa na Serikali ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (DARUSO).
04
Baadhi ya wahudhuriaji wakishangilia moja ya onesho lililokuwa likifanywa na mmoja wa wachekeshaji mahiri kutoka Kenya, Erick Omondi katika hafla iliyoandaliwa mwishoni mwa juma lililopita na Serikali ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (DARUSO) na kudhaminiwa na Benki ya NBC yenye lengo la kuwasaidia wanafunzi wanaoshindwa kuendelea na masomo kutokana na kushindwa kumudu gharama za ada chuoni hapo. 
01
Meneja wa Benki ya NBC Tawi la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Bw. Emmanuel Mapunda (katikati) akisalimiana na Rais wa Serikali ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (DARUSO) Bw. Hamis Mussa katika hafla ya kuchangisha fedha kwa njia ya vichekesho na burudani iitwayo ‘Cheka Nisome’ iliyodhaminiwa na NBC yenye lengo la kuwasaidia wanafunzi wanaoshindwa kuendelea na masomo kutokana na kushindwa kumudu gharama za ada. Hafla hiyo ilifanyika chuoni hapo jijini Dar es Salaam juzi. Kulia ni Meneja Chapa na Mawasiliano wa NBC Bw. David Raymond.02
Meneja Chapa na Mawasiliano wa Benki ya NBC Bw. David Raymond (kulia), akisalimiana na Rais wa Serikali ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (DARUSO) Bw. Hamis Mussa katika hafla ya kuchangisha fedha kwa njia ya vichekesho na burudani iitwayo ‘Cheka Nisome’ iliyodhaminiwa na NBC yenye lengo la kuwasaidia wanafunzi wanaoshindwa kuendelea na masomo kutokana na kushindwa kumudu gharama za ada. Hafla hiyo ilifanyika chuoni hapo jijini Dar es Salaam juzi. Katikati ni Meneja wa NBC Tawi la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Bw. Emmanuel Mapunda.

No comments:

Post a Comment

Benki ya Biashara DCB kuendelea kuboresha Maisha ya Watanzania

Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Biashara ya DCB, Bi. Zawadia Nanyaro (wa nne kulia) akishikana mikono na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Bias...

Pages