MCHIMBAJI MDOGO WA TANZANITE AIBUKA NA MAWE YENYE THAMANI YA SH. BILIONI 7.8. - Business Insights

Mgongopr.blogspot.com is a business centered online platform highlighting trade, finance and economic news in Tanzania. Our coverage is customised to ensure we consolidate brands, boost sales and nurture investments. The site is an imprint of Mgongo Logistics and Solutions, a trusted consultancy firm, offering Social Media Management, Photography, Videography, Advertising, Event Management and Translation. For more information contact us via; Phone: +715765454 email: mgongo@gmail.com

Breaking

Wednesday, June 24, 2020

MCHIMBAJI MDOGO WA TANZANITE AIBUKA NA MAWE YENYE THAMANI YA SH. BILIONI 7.8.


Mchimbaji mdogo wa madini ya Tanzanite Bw. Saniniu Laizer  bilionea mpya Tanzania aliefanikiwa kupata Mawe mawili makubwa ya Tanzanite yenye dhamani ya Sh. Bilioni 7.8
Mawe makubwa mawili ya Tanzanite moja lina kilo 9.2 ambalo lina thamani ya shilingi bilioni 4.5 na la pili lina kilo 5.8 lenye thamani shilingi bilioni 3.3.
Afisa Madini akionyesha moja ya jiwe la Tanzanite lilipatikana

Katibu Mkuu Wizara ya Madini Profesa Simon Msanjila amesema  kuwa leo Wizara inamtabua Mchimbaji mdogo wa madini ya Tanzanite Bw. Saninniu Laizer kuwa bilionea baada ya kupata  mawe makubwa mawili yenye thamani ya shilingi bilioni 7.8.

Katibu Mkuu amesema kuwa mchimbaji huyo amepata mawe hayo mawili ambapo moja lina kilo 9.2 ambalo lina thamani ya shilingi bilioni 4.5 na la pili lina kilo 5.8 lenye thamani shilingi bilioni 3.3.

"Na utofauti wake ni kwamba mawe ya uzito huo hayajawahi kupatikana kwenye machimbo ya tanzanite tangu machimbo yaanze na yamepatikana ndani ya ukuta wa Mirereni kwahiyo hii ni rekodi mpya ya kupata mawe yenye uzito huo" amesema Prof. Msanjila

Profesa Msanjila amesema kuwa sekta ya madini inauwezo wa kumfanya mtu kuwa bilionea kwa haraka, ameongeza kuwa kunahitaji kuwa uwekezaji wa dhati katika sekta hiyo.

No comments:

Post a Comment

ABSA BANK TANZANIA STRENGTHENS PARTNERSHIPS WITH CORPORATE CLIENTS THROUGH NETWORKING BREAKFAST

Absa Group Chief Executive Officer for Corporate and Investment Banking (CIB), Mr. Zaid Moola (second right), engages with some of Absa Bank...

Pages