RC MAKALLA AWATAKA WAFANYABIASHARA KUTORUDI NA KUFANYA BIASHARA KWENYE MAENEO WALIYOHAMA - Business Insights

Mgongopr.blogspot.com is a business centered online platform highlighting trade, finance and economic news in Tanzania. Our coverage is customised to ensure we consolidate brands, boost sales and nurture investments. The site is an imprint of Mgongo Logistics and Solutions, a trusted consultancy firm, offering Social Media Management, Photography, Videography, Advertising, Event Management and Translation. For more information contact us via; Phone: +715765454 email: mgongo@gmail.com

Breaking

Tuesday, November 2, 2021

RC MAKALLA AWATAKA WAFANYABIASHARA KUTORUDI NA KUFANYA BIASHARA KWENYE MAENEO WALIYOHAMA

 
  • Asema Serikali itatumia sheria kuyalinda maeneo hayo na kurudi kufanya biashara katika maeneo hayo ni kosa.
  • Awataka Wamachinga wengi Wajitokeze kupata nafasi Machinga complex.
  • Atangaza nafasi 2,000 na route Za magari ya Kariakoo kufika machinga complex na masoko mengine mkoani  DSM.
  • Asema zoezi hili ni endelevu.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Amos Makalla amesema Katika kuyalinda maeneo walipoondoka Machinga Serikali itatumia Sheria kwa Wote walioondoa Vibanda na kufanya Biashara Chini.

Akizungumza wakati wa ziara ya kutembelea Maeneo mbalimbali walipohamia Machinga kukagua changamoto ili Serikali izitatue, RC Makalla amewataka Wafanyabiashara waliokuwa Kariakoo, Karume, Msimbazi na Katika ya mji kufika Machinga Complex ili wapatiwe nafasi ambapo mpaka Sasa nafasi zilizosalia ni 2,100.
RC Makalla pia amewaelekeza Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi kuanza rasmi zoezi la Usafi kwenye maeneo yote walipoondoka Machinga na kuhakikisha yanalindwa yasivamiwe upya.

Aidha RC Makalla amesema Serikali itaendelea kufanyia kazi changamoto zote zitakazoonekana kwenye maeneo walipopelekwa ili Biashara zifanyike na Wafanyabiashara wapate kipato.
Kwa mujibu wa sheria za miji na majiji zinaeleza kuwa kufanya biashara kwenye maeneo yaliyokatazwa ni kosa kisheria ambapo adhabu kwa anaefanya kosa hilo ni kifungo Cha mwaka mmoja na faini ya Shilingi laki tatu.

No comments:

Post a Comment

ABSA BANK TANZANIA STRENGTHENS PARTNERSHIPS WITH CORPORATE CLIENTS THROUGH NETWORKING BREAKFAST

Absa Group Chief Executive Officer for Corporate and Investment Banking (CIB), Mr. Zaid Moola (second right), engages with some of Absa Bank...

Pages