WATENDAJI WA BENKI YA ABSA TANZANIA WALIVYOSHIRIKI KIKAO CHA BAJETI JIJINI DODOMA JANA - Business Insights

Mgongopr.blogspot.com is a business centered online platform highlighting trade, finance and economic news in Tanzania. Our coverage is customised to ensure we consolidate brands, boost sales and nurture investments. The site is an imprint of Mgongo Logistics and Solutions, a trusted consultancy firm, offering Social Media Management, Photography, Videography, Advertising, Event Management and Translation. For more information contact us via; Phone: +715765454 email: mgongo@gmail.com

Breaking

Friday, June 12, 2026

WATENDAJI WA BENKI YA ABSA TANZANIA WALIVYOSHIRIKI KIKAO CHA BAJETI JIJINI DODOMA JANA

 

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (katikati), akipozi kwa picha ya kumbukumbu na Ofisa Mkuu wa Fedha wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Bernard Tesha (kushoto), na Mkuu wa Mikakati na Data wa benki hiyo, Bw. John Mosha, ndani ya viwanja vya bunge, mara baada ya mheshimiwa waziri, kuwasilisha bajeti ya serikali ya Sh 63.2 trilioni, itakayotumika katika Mwaka 2026/2027, bungeni, jijini Dodoma, jana.
Ofisa Mkuu wa Fedha wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Bernard Tesha (kulia), Mkuu wa Mikakati na Data wa benki hiyo, Bw. John Mosha (wa tatu kulia), pamoja na baadhi ya wawakilishi kutoka taasisi za fedha, wakimsikiliza kwa makini, Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar, wakati akiwasilisha bajeti ya serikali ya Sh 63.2 trillioni, itakayotumika katika Mwaka 2026/2027, bungeni, jijini Dodoma, jana.
Ofisa Mkuu wa Fedha wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Bernard Tesha (kulia, mstari wa nyuma) na Mkuu wa Mikakati na Data wa benki hiyo, Bw. John Mosha (wa tatu kulia, mstari wa nyuma), pamoja na baadhi ya wawakilishi kutoka taasisi za fedha, wakisimama kwa utambulisho, kabla Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar, hajawasilisha bajeti ya serikali ya Mwaka 2026/2027, bungeni, jijini Dodoma, jana.
Ofisa Mkuu wa Fedha wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Bernard Tesha (wa tatu kushoto), akibadilishana mawazo na baadhi ya wawakilishi kutoka taasisi mbalimbali waliohudhuria uwasilishwaji wa bajeti ya serikali ya Mwaka 2026/2027, bungeni, jijini Dodoma, jana, uliofanywa na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Ndege la Air Tanzania Company Limited (ATCL) Mhandisi Peter Ulanga (Katikati), akipiga picha ya kumbukumbu na Ofisa Mkuu wa Fedha wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Bernard Tesha (kulia kwake) na Mkuu wa Mikakati na Data wa benki hiyo, Bw. John Mosha, ndani ya viwanja vya bunge, muda mfupi baada ya Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar, kuwasilisha bajeti ya serikali ya Mwaka 2026/2027, bungeni, jijini Dodoma, jana.

No comments:

Post a Comment

Absa Bank Tanzania Showcases Innovative Banking Solutions at Nane Nane 2026

  Minister for Agriculture, Hon. Daniel Chongolo (centre), receives an explanation about various banking services offered by Absa Bank Tanza...

Pages