Friday, May 19, 2017
Brazuka Kibenki kutimua vumbi Julai
Mwakilishi wa Benki ya
Barclays, Rajabu Abdallah (kulia), akichagua tiketi katika hafla ya utambulisho
wa Ligi ya Mabenki iliyopewa jina la ‘Brazuka Kibenki’ itakayoshirikisha timu
za mpira wa miguu na kikapu kutoka katika benki zaidi ya 16 zajijini Dar es
Salaam. Ligi hiyo inatarajiwa kuanzia tarehe 01- julai mwaka huu. Hafla ya
utambulisho wa ligi hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam hivi karibuni.iKushoto ni baadhi ya wawakilishi wa benki hizo; Richard
Mwalwiba wa NMB, na Mratibu wa mashindano hayo Raymond
Bunyinyiga.
Mwakilishi wa Benki ya
UBA,Vitalis Bosha (kulia), akichagua tiketi katika hafla ya utambulisho wa Ligi
ya Mabenki iliyopewa jina la ‘Brazuka Kibenki’ itakayoshirikisha timu zampira
wa miguu kutoka katika benki zaidi ya 16 zajijini Dar es Salaam. Kushoto ni
baadhi ya wawakilishi wa benki hizo; Mratibu wa mashindano hayo
Raymond Bunyinyiga na Iddi Yakoub wa DTB.
Mratibu na Mwanzilishi wa
Ligi ya Mabenki iliyo pewa jina la Brazuka Kibenki Raymond Bunyinyiga wa pili
(kushoto) akizungumza na waandishi wa habari katika hafla ya utambulisho wa
Ligi ya Mabenki iliyopewa jina la ‘Brazuka Kibenki’ itakayoshirikisha timu
zampira wa miguu kutoka katika benki zaidi ya 16 zajijini Dar es Salaam. Ligi
hiyo inatarajiwa kuanzia tarehe 01- julai mwaka huu. Hafla ya utambulisho wa
ligi hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam jana. Wengine pichani ni baadhi ya
wawakilishi wa Benki hizo.
Mratibu na Mwanzilishi wa
Ligi ya Mabenki ya Brazuka Kibenki, Raymond Bunyinyiga wa pili (kztikati) akizungumza na waandishi wa habari katika hafla ya
utambulisho wa ligi hiyo. kushoto ni mwakilishi wa Benki ya NMB, Richard
Mwalwiba na mwakilishi wa DTB, Iddi Yakoub.
Mwakilishi na timu kampeni
wa Benki ya Barclays Tanzania Rajabu Abdallah (wa tatu kushoto) akizungumza na waandishi wa
habari katika hafla hiyo. Kushoto ni baadhi ya wawakilishi wa benki hizo;
Raymond Bunyinyiga wa Barclays, Iddi Yakoub wa DTB, mwakilishi wa Exim Benki
Mikidadi Ngoma (kulia) na wa pili kulia ni Richard Mwalwiba kutoka NMB.
Mwakilishi na timu
kampeni wa Benki ya Exim,Mikidadi Ngoma wa tatu
(kushoto) akizungumza na waandishi wa habari katika hafla ya utambulisho
wa Ligi ya Brazuka Kibenki jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Wengine kutoka kushoto ni baadhi ya
wawakilishi wa benki hizo; Raymond Bunyinyiga Barclays, Iddi Yakoub wa DTB, mwakilishi wa Exim Benki, Mikidadi Ngoma (kulia) na wa pili kulia ni Richard Mwalwiba wa NMB.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Absa Dar City Marathon 2024 zatimua vumbi jijini Dar es Salaam
Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Absa Tanzania, Bwana Aron Luhanga (kushoto), akikabidhi zawadi kwa mshindi wa kwanza wa mbio za nu...
No comments:
Post a Comment