NBC yadhamini maadhimisho ya Siku ya Vicoba nchini - THINKING IN BUSINESS

Mgongopr.blogspot.com is a business centered online platform highlighting trade, finance and economic news in Tanzania. Our coverage is customised to ensure we consolidate brands, boost sales and nurture investments. The site is an imprint of Mgongo Logistics and Solutions, a trusted consultancy firm, offering Social Media Management, Photography, Videography, Advertising, Event Management and Translation. For more information contact us via; Phone: +255 767765454, email: mgongo@gmail.com

Breaking

Sunday, October 15, 2017

NBC yadhamini maadhimisho ya Siku ya Vicoba nchini

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage (wa pili kushoto), akisalimiana na Mkuu wa Bidhaa na Wateja Rejareja wa Benki ya NBC, Andrew Lyimo alipokwenda kuzindua rasmi maadhimisho ya Siku ya Vicoba nchini katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam jana ambayo NBC ilikuwa ni mmoja wa wadhamini ambapo ilizindua akaunti maalumu ya kikundi iitwayo ‘NBC Kikundi Account’ ili kuwawezesha watanzania kiuchumi. Akaunti inafunguliwa na  watu kuanzia watano na kuendelea. Wengine kutoka kushoto ni, Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji (NEEC), Beng`i Mazana Issa, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Wanawake Tanzania (TWB), Japhet Justine, Mkurugenzi wa Mifuko ya Uwezeshaji Baraza la Taifa la Uwezeshaji (NEEC), Edwin Christant na Mkurugenzi wa Uwezeshaji Baraza la Taifa la Uwezeshaji (NEEC), Anna Dominick.
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage (kulia), akimsikiliza Meneja Bidhaa za Uwekezaji wa NBC, Dorothea Mabonye (wa pili kushoto), huku wenzake wakiangalia wakati akitembelea banda la NBC katika maadhimisho hayo.  
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage (kulia), akisalimiana na Ofisa Mauzo wa Benki ya NBC, Witness Leverian alipokwenda kuzindua rasmi maadhimisho ya Siku ya Vicoba nchini katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam jana. NBC ilikuwa ni kati ya wadhamini wa maadhimisho hayo ambapo imezindua akaunti maalumu ya kikundi iitwayo ‘NBC Kikundi Account’ ili kuwawezesha watanzania kiuchumi katika kikundi cha watu kuanzia watano na kuendelea.
Ofisa Mauzo wa Benki ya NBC, Witness Leverian (kulia), akitoa maelezo kuhusu huduma na bidhaa za benki hiyo kwa baadhi ya washiriki wa maonyesho ya maadhimisho ya Siku ya Vicoba nchini katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam jana.
Ofisa Mauzo wa Benki ya NBC, Rosina Simbila (kushoto), akitoa maelezo kuhusu huduma na bidhaa za benki hiyo kwa baadhi ya washiriki wa maonyesho ya maadhimisho ya Siku ya Vicoba nchini katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam jana.
Ofisa Mauzo wa Benki ya NBC, Stephen Ngereza (kulia), akitoa maelezo kuhusu huduma na bidhaa za benki hiyo kwa baadhi ya washiriki wa maonyesho ya maadhimisho ya Siku ya Vicoba nchini katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam jana.

No comments:

Post a Comment

ABSA BANK TANZANIA REAFFIRMS COMMITMENT TO SUPPORTING TANZANIA’S HEALTH SECTOR

Absa Bank Tanzania Managing Director, Obedi Laiser (right), competes alongside other participants during the 10-kilometre race of the 2026 A...

Pages