Wakazi wa jiji la Dar es Salaam, watakiwa kujenga mazoea ya kunawa mikono. - THINKING IN BUSINESS

Mgongopr.blogspot.com is a business centered online platform highlighting trade, finance and economic news in Tanzania. Our coverage is customised to ensure we consolidate brands, boost sales and nurture investments. The site is an imprint of Mgongo Logistics and Solutions, a trusted consultancy firm, offering Social Media Management, Photography, Videography, Advertising, Event Management and Translation. For more information contact us via; Phone: +255 767765454, email: mgongo@gmail.com

Breaking

Wednesday, January 31, 2018

Wakazi wa jiji la Dar es Salaam, watakiwa kujenga mazoea ya kunawa mikono.

Afisa Afya Wilaya kinondoni John Kijumbe akizungumza na waandishi wa habari leo katika hafla yakufunga mradi wa magonjwa ya kuambukiza kwa kunawa mikono (kutoka kushoto) ni Mratibu wa Mradi huo Rose Temu, Mganga Mkuu  wa Kituo cha Afya Magomeni Omari Mwanga, na  ni Afisa Elimu Sayansikimu na Afya Manispaa ya Kinondoni Martha Kussaga. hafla hiyo imefanyika kashule ya Msingi Kigogo
Afisa Elimu Sayansikimu na Afya Manispaa ya Kinondoni Martha Kussaga. (kulia) akizungumza na waandishi wa habari leo katika hafla yakufunga mradi wa magonjwa ya kuambukiza kwa njia ya kunawa mikono, (kutoka kushoto) ni Mratibu wa Mradi huo Rose Temu, Mganga Mkuu  wa Kituo cha Afya Magomeni Omari Mwanga, na Afisa Afya Wilaya kinondoni John Kijumbe, hafla hiyo imefanyika kashule ya Msingi Kigogo
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya Msingi Kigogo wakiwa katika hafla hiyo Picha na Brian Peter

Wananchi wametakiwa kunawa mikono wakati wote kabla ya kula ili kuepuka magonjwa ya milipuko yatokanayo na maradhi kutokunawa mikono. 

Akizungumza na waandishi wa habari Leo katika hafla ya kufunga Mradi  wa magonjwa wa kuambukiza kwa njia ya kunawa mikono jijini Dar es Salaam Afisa Afya Wilaya kinondoni JOHN KIJUMBE amesema walianzisha Mradi wa Kunawa mikono Uliofadhiliwa na shirika la  kimataifa kutoka Japan JICA,likishirikiana na kituo cha  Afya Magomeni ukiwa na lengo la kutoa elimu ya kujikinga na maradhi ya kuambukiza kwa Njia ya kunawa mikono .

Amesema Mardi huo ulianzishwa Julai na kuzinduliwa Septemba 25,2017  ambapo umekamili January 2018 ambapo ulilenga kutoa elimu ya kuanawa mikono mashuleni katika Wilaya ya Kinondoni ambapo waliweza kutoa elimu hiyo kwa wanafunzi pamoja na walimu na kubaini kuwa wananchi wanauelewa mdogo wa Kunawa mikono baada ya kutoka chooni,na kabla ya kula.

"Katika huu mradi tuliouanzisha chini ya shirika la kimataifa la Japan (JICA) likishirikiana na kituo cha Afya Magomeni tumeweza kutoa elimu kwa shule katika Wilaya ya Kinondoni  na kubaini kuwa wanafunzi wengi hawana elimu ya kunawa mikono jambo ambalo ni hatari kwa Afya zao na kusababisha magonjwa ya Milipuko "Amesema Kijumbe. 

Aidha amebainisha changamoto walizokumbana nazo ambapo amesema watu wanachukulia kunawa mikono siyo jambo  muhimu, pamoja na ukosefu wa vifaa vya kunawa mikono katika jamii na mashuleni pia, hivyo amesema mradi huo utakuwa ni endelevu kwa jamii ili kuweza kukuza elimu hiyo ya kunawa mikono. 

Pia amesema katika mradi huo wamepata mafanikio mbalimbali ambapo wameweza kufunga vifaa vya kunawia mikono kwa baadhi ya shule.

Kwa upande wake mratibu wa Mradi huo Rose Temu amesema Mradi huo utakuwa emdelevu na kutoa wito kwa watanzania kujenga mazoea ya kunawa mikono unapotoka chooni na  kabla ya kula ili kuepuka magonjwa ya milipuko.

No comments:

Post a Comment

APeF Yazindua Mfuko wa Ziada Kupanua wigo wa uwekaji Akiba, Uwekezaji na Ulinzi

  Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana, (CMSA), CPA Nicodemus Mkama, akikabidhi waraka wa ofa kwa Kaimu Mwenyekiti ...

Pages