RC MAKONDA AKUTANA NA BALOZI WA UFARANSA - Serious Business

Mgongopr.blogspot.com is a serious online platform of business and finance news from around Tanzania. We are a trusted site covering the entire spectrum, from small enterprises to large businesses entities. For photography, videography, media management, events management, advertising, public relations, translation, interpreters, and more services, please contact us: MPP Ltd phone: +255 767765454, email: mgongo@gmail.com

Breaking

Thursday, April 12, 2018

RC MAKONDA AKUTANA NA BALOZI WA UFARANSA

23

Mkuu wa mkoa Dar es salaam Paul Makonda amekutana na Balozi wa Ufaransa nchini na kujadili kuhusu kongamano la uchumi litakalofanyika mapema jumatatu wiki ijayo.

Akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam Rc Makonda amemshukuru balozi huyo na kueleza kuwa wamekuwa marafiki wazuri na Serikali ya Tanzania.
werAidha kuuhusu kongamano hilo Makonda amesema siku ya jumatatu makampuni 30 kutoka Ufaransa yatawasili nchini na kufanya mkutano wenye malengo ya kulifanya jiji la Dar es salaam kuwa kama majiji mengine duniani katika masuala ya maji, afya, usafiri na masuala mengine ya kiteknolojia.

Ameeleza kuwa makampuni hayo yataangalia fursa na vipaumbele vya serikali watakavyovitumia katika kuleta maendeleo na ametoa rai kwa wafanyabiashara wa jiji la Dar es salaam kuja katika ofisi za Mkuu wa Mkoa kujifunza na kuunganishwa na wafanyabiashara hao kutoka ufarasa ili waweze kujifunza na kujenga urafiki katika masoko ya bidhaa zao.

Naye Balozi wa Ufaransa nchini Federic Clavier amefurahi na kumshukuru mkuu ya Mkoa Dar na kueleza kuwa Dar ni mji unaoendelea kukua kiuchumi sambamba na dhamira ya Rais Magufuli ya kufikia uchumi wa kati kufikia mwaka 2025.

Amesema mkutano huo utakuwa na faida baina ya nchi hizi mbili hasa katika kubadilishana teknolojia katika sekta mbalimbali hasa kwa kuangalia afya, maji pamoja na miundombinu na amehaidi matokeo mazuri yenye faida kwa nchi hizo.
11Kuhusu zoezi la kusaidia watoto waliotelekezwa Makonda amewashukuru wanahabari kwa kuwa sehemu ya wapatanishi wa familia hizo aidha amewataka wananchi kuja kupata huduma katika viwanja vya ofisi yake na sio katika simu na mitandao na ameeleza kuwa hadi sasa familia 178 wameelewana na kukubaliana kupeana fedha za matunzo na zaidi ya watu 1498 wameshapatiwa huduma na siku ya jumatatu wataitwa baba wa familia hizo licha ya baadhi yao kuanza kuripoti na ameeleza kuwa walio tayari kupima DNA wajitokeze watakaokaidi watachukuliwa hatua za kisheria.

No comments:

Post a Comment

  International forum poised to open up AFRICA - ASIAN economies to the world   By Peter Mgongo Dar es Salaam, Tanzania 29th April, 2024...

Pages