Monday, May 28, 2018
RESPECT BARBER SHOP IMEANDAA FUTARI KWA WAKAZI WA DAR
Ukizungumzia moja ya mameneja wenye majina makubwa kwenye tasnia ya muziki wa Bongo Fleva na Dansi hapa nchini, huwezi kuacha kutaja jina la Mohamed Kiumbe ‘Chief kiumbe’ jana amefuturisha jijini Dar es salaam katika ofisi za Respect Barber Shop Kinondoni ambapo mamia ya watu walihudhuria katika futari hiyo wakiwemo wasanii. mbalimbali wa bongofleva na filamu.
Pia Respect Barber Shop imeamua kuandaa futari hiyo kwa wakazi wa jiji hilo ili kuonesha upendo pia kama moja ya sadaka katika mwezi huu mtukufu wa ramadhani.
Baadhi ya wasanii waliohudhuria Iftari hiyo ni pamoja na Khadija Kopa, Mwajuma Abdul ‘Queen Darling’ na Bonge la Nyau na wengine wengi wakiwepo wasanii wa dansi.
Akizungumza na waandishi wa habari kwenye Iftari hiyo, Msemaji wa saluni ya Respect, Dakota Delavida amesema kuwa huu ni mwanzo tu ila Mungu akiwapa uzima wataongeza wigo wao kwani ni kitendo cha kurudisha fadhila kwa jamii.
“Chakula ni sadaka na huwezi kupanga kiishie hapa tulijipanga vya kutosha, hii ni mara yetu ya kwanza mwenyezi Mungu akitujaalia uzima tutafanya tukio kama hili tena kwani ni kurudisha fadhili kwa jamii tunayoihudumia” alisema Dakota.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Benki ya Absa Tanzania na ASA Microfinance Yaadhimisha Miaka Minne ya Mafanikio katika Kuwawezesha Wanawake na Kubadilisha Jamii
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (Katikati), akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo,...


No comments:
Post a Comment