Majaliwa kuwa mgeni rasmi mashindano ya kimataifa ya kuhifadhi Kuruan - THINKING IN BUSINESS

Mgongopr.blogspot.com is a business centered online platform highlighting trade, finance and economic news in Tanzania. Our coverage is customised to ensure we consolidate brands, boost sales and nurture investments. The site is an imprint of Mgongo Logistics and Solutions, a trusted consultancy firm, offering Social Media Management, Photography, Videography, Advertising, Event Management and Translation. For more information contact us via; Phone: +255 767765454, email: mgongo@gmail.com

Breaking

Friday, June 1, 2018

Majaliwa kuwa mgeni rasmi mashindano ya kimataifa ya kuhifadhi Kuruan

1%2B%25281%2529

ddddddddddd



WAZIRI Mkuu Kasim Majaliwa anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika fainali za  Mashindano  makubwa  ya 26 ya Kusoma na Kuhifadhi Kuruan Tukufu Duania.

Mbali na majaliwa, viongozi wengine watakaohudhuria fainali hizo zitakazofanyika katika ukumbi wa Diamond  DiamondJubilee, kesho,  jijini Dar es salaam ni  marais wastaafu, Ali Hassan Mwinyi na Dk. Jakaya Kikwete na Makamu wa Rais Mstaafu Dk. Mohammed Gharib Bilal

Akizungumza jijini na waandishi wa habari,, Mratibu wa mashindano hayo,  Sheikh Mohammed  Nasoro,  kutoka Taasisi ya Kuhifadhisha Kuruan TukufuTanzania ambao ndiyo wandaaji wa mashindano hayo,   amesema jumla ya nchi18 zitashiriki.

 Amezitaja baadhi ya nchi hizo kuwa ni Tanzania, Saud Arabia, Mali, Uganda, Kenya, Afrika Kusini, Malawi, Congo DRC,  Russia, Sylia, Yemen, Malaysia, Bangladesh, Uingereza, na Burundi.

“Washiriki wote wamewasili nchini  ambapo juzi na jana tuliwafanyia mashindano ya mwisho ya kupata wale bora ambao wataingia katika fainali kesho,”alisema Sheikh  Nasoro.
Alisema, majaji watatoka nchi za Uingereza, Yemen, Saud Arabia  na Sudan na tayari wamewasili nchini.

“Zawadi tutatangaza baadaye ingawa pia fainali hizo zitakwenda sambamba na utoaji wa tuzo za heshima  kwa watu mbalimbali,”alibainisha.

Katibu wa Taasisi ya Kuhifadhisha Kuruan Tukufu Tanzania, Mohammed Ally Hassan, amewaomba watanzania kushiriki kwa wingi kwani jambo hilo ni la kheri hasa katika kipindi hiki cha Ramadhan.

Akizungumza kwa niaba ya jopo la majaji wa fainali hizo, Jaji Dk. Abbas Hamza kutoka nchini Sudan , amesema wanaamini haki itatendeka na kuwataka watanzania kuhudhuria kwa wingi.

No comments:

Post a Comment

SERIKALI YASISITIZA UTAALAMU NA UBUNIFU KATIKA UNUNUZI NA UGAVI

Serikali imewataka wataalam wa ununuzi na ugavi nchini kuongeza ubunifu, uongozi bora na matumizi ya teknolojia za kisasa ili kuongeza ufani...

Pages