Wednesday, September 4, 2019
 
Home
LOCAL
Taasisi ya SAP kupitia program ya INITIATIVE CODE WEEKS imeanza kutoa mafunzo ya Programming kwa walimu
Taasisi ya SAP kupitia program ya INITIATIVE CODE WEEKS imeanza kutoa mafunzo ya Programming kwa walimu
Mkurugenzi Ushirika na Uwajibikaji wa Jamii EMEA na Mkuu wa wiki ya Code Afrika, Claire Gillissen (kulia), akizungumza na Walimu kutoka shule mbalimbali wakati wa uzinduzi wa kutoa  mafunzo ya Programming  kwa walimu kutoka Tanzania na Afrika nzima  yenyelengo la kukuza elimu mashuleni na  na jamii nzima. uzinduzi huo umefanyika  leo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa SAP, Liam Ryan, akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa kutoa  mafunzo ya Programming  kwa walimu kutoka Tanzania na Afrika nzima  yenyelengo la kukuza elimu mashuleni na  na jamii. Uzinduzi huo umefanyika  leo jijini Dar es Salaam.
Afisa Miradi wa taasisi ya Apps and Girls, Jesca Mmari, akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa kutoa  mafunzo ya Programming  kwa walimu kutoka Tanzania na Afrika nzima  yenyelengo la kukuza elimu mashuleni na  na jamii. Uzinduzi huo umefanyika  leo jijini Dar es Salaam.
Mwalimu wa shule ya Sekondari ya Benjamini Mkapa akizungumza katika haflahiyo.
Kutokana na umuhimu wa teknolojia katika elimu na jamii  kiujumla kuongezeka,Kutokana na umuhimu wa teknolojia katika elimu na jamii  kiujumla kuongezeka,Taasisi ya SAP kupitia program ya INITIATIVE CODE WEEKS imeanza kutoa mafunzo  ya  Programming kwa walimu  kutoka Tanzania na Afrika nzima kwa lengo la kuwafikia wanafunzi wengi na kutengeneza msingi mzuri wa teknolojia kwa kizazi cha baadae.
Akizungumza  leo jijini Dar es salaam wakati wa uzinduzi wa mafunzo hayo Mkurugenzi Mkuu wa SAP, Liam Ryan amesema kuwa SAP ikishirikiana na taasisi mbalimbali wamemekusudia kwa dhati kutoa mafunzo kwa walimu zaidi ya mia tano kutoka Tanzania na zaidi ya walimu elfu tano kutoka Afrika wakiwa na lengo la kuwafikia wanafunzi na watoto zaidi ya milioni moja na nusu Afrika nzima.
Kwa upande wake Afisa Miradi wa taasisi ya Apps and Girls, Jesca Mmari amesema kuwa wanakusudia kuwafundisha walimu programu iitwayo scratch ambayo itatoa hamasa  na hamu ya wanafunzi kupenda kujifunza teknolojia ambpo amewataka walimu walioko kwenye mafunzo hayo wapende na  wajitume kujifunza  kuhusu programu hiyo na  teknolojia kwa ujumla ili waweze kuwafundisha wanafunzi kikamilifu.
Akizungumza mmoja wa walimu  katika mafunzo hayo,Mussa  Awadhi kutoka shule ya sekondari Benjaminj Mkapa, amesema kuwa programu  ya scratch inamuwezesha mwanafunzi kuelewa kwa urahisi masuala ya teknolojia kwani imetengenezwa kwa mfumo wa picha  (katuni)na ni rahisi kujifunzia. imeanza kutoa mafunzo  ya  Programming kwa walimu  kutoka Tanzania na Afrika nzima kwa lengo la kuwafikia wanafunzi wengi na kutengeneza msingi mzuri wa teknolojia kwa kizazi cha baadae.
Akizungumza  leo jijini Dar es salaam wakati wa uzinduzi wa mafunzo hayo Mkurugenzi Mkuu wa SAP, Liam Ryan amesema kuwa SAP ikishirikiana na taasisi mbalimbali wamemekusudia kwa dhati kutoa mafunzo kwa walimu zaidi ya mia tano kutoka Tanzania na zaidi ya walimu elfu tano kutoka Afrika wakiwa na lengo la kuwafikia wanafunzi na watoto zaidi ya milioni moja na nusu Afrika nzima.
Kwa upande wake Afisa Miradi wa taasisi ya Apps and Girls, Jesca Mmari amesema kuwa wanakusudia kuwafundisha walimu programu iitwayo scratch ambayo itatoa hamasa  na hamu ya wanafunzi kupenda kujifunza teknolojia ambpo amewataka walimu walioko kwenye mafunzo hayo wapende na  wajitume kujifunza  kuhusu programu hiyo na  teknolojia kwa ujumla ili waweze kuwafundisha wanafunzi kikamilifu.
Akizungumza mmoja wa walimu  katika mafunzo hayo,Mussa  Awadhi kutoka shule ya sekondari Benjaminj Mkapa, amesema kuwa programu  ya scratch inamuwezesha mwanafunzi kuelewa kwa urahisi masuala ya teknolojia kwani imetengenezwa kwa mfumo wa picha  (katuni)na ni rahisi kujifunzia.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Benki ya Absa Tanzania na ASA Microfinance Yaadhimisha Miaka Minne ya Mafanikio katika Kuwawezesha Wanawake na Kubadilisha Jamii
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (Katikati), akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo,...
 
 
 Posts
Posts
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment