Tuesday, November 5, 2019
Home
LOCAL
MSANII DIAMOND PLATNUMZ NA WASAFI MEDIA WAMUUNGA MKONO RC MAKONDA KAMPENI YA UPASUAJI WA MOYO KWA WATOTO KUTOKA FAMILIA DUNI
MSANII DIAMOND PLATNUMZ NA WASAFI MEDIA WAMUUNGA MKONO RC MAKONDA KAMPENI YA UPASUAJI WA MOYO KWA WATOTO KUTOKA FAMILIA DUNI
Kampeni ya ufadhili wa matibabu
ya Upasuaji wa Moyo kwa Watoto 60 kwa muda wa miezi sita iliyoanzishwa na Mkuu
wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda mevuka malengo kutoka Watoto 60 hadi
kufikia watoto 90 ikiwa ni ongezeko la watoto 30 jambo linalokwenda kurejesha
uhai kwa watoto hao ambao tayari wazazi wao walikuwa wamekata tamaa kutokana na
kushindwa kumudu gharama za matibabu.
RC Makonda amesema ongezeko
hilo la Watoto 30 limetokana na Kampeni ya uchangishaji wa fedha iliyofanywa na
Kituo cha Utangazaji cha Wasafi Media ambao wamefanikiwa kuchangisha kiasi cha
Shilingi milioni 60 ambapo kati ya fedha hizo Shilingi Milioni 20 zimetolewa na
msanii Diamond na nyingeni zimetolewa na wadau na wasanii mbalimbali wakiwemo
Mbosso, Rayvany, Lavalava, Irine Uwoya, Queen Darling, Babutale, Jux, Star
Times, DSTV na wadau wengine walioguswa na jambo hilo.
Aidha RC Makonda amemshukuru
msanii Diamond kwa kujitolea 20% ya mapato yote yatakayopatikana kupitia
tamasha la Wasafi Festival 2019 yatumike kugharamia matibabu ya moyo kwa Watoto
waliolazwa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete.
Kwa upande wake Msanii Nasib
Abdul almaarufu Kama Diamond Plutnumz amempongeza RC Makonda kwa kuwa kiongozi
mwenye Moyo wa Kujali na kubeba changamoto za wananchi anaowaongoza.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Benki ya Biashara DCB kuendelea kuboresha Maisha ya Watanzania
Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Biashara ya DCB, Bi. Zawadia Nanyaro (wa nne kulia) akishikana mikono na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Bias...
No comments:
Post a Comment