BIMA YA AFYA SASA NI KWA KILA MTU - NHIF - Serious Business

Mgongopr.blogspot.com is a serious online platform of business and finance news from around Tanzania. We are a trusted site covering the entire spectrum, from small enterprises to large businesses entities. For photography, videography, media management, events management, advertising, public relations, translation, interpreters, and more services, please contact us: MPP Ltd phone: +255 767765454, email: mgongo@gmail.com

Breaking

Monday, September 28, 2020

BIMA YA AFYA SASA NI KWA KILA MTU - NHIF

Mkuu wa Wilaya ya Geita Fadhil Juma akimkabidhi kitambulisho Cha Toto Afya Kadi kwa mmoja wa Watoto waliojiunga na bima ya afya kwenye hafla ya makabidhiano yaliyofanyika  kwenye Banda la Mfuko wa bima ya afya (NHIF).

Mkuu wa wilaya ya Geita Fadhil Juma akiwa katika picha ya pamoja na Watoto na wazazi waliojiunga na Toto Afya Kadi baada ya kuwakabidhi kadi zao.

Meneja wa Mfuko wa bima ya afya Mkoa wa Geita Elius Odhiambo akimkabidhi mkuu wa Wilaya ya Geita Fadhil Juma Tshert ya NHIF baada ya kukabidhi kadi za toto afya kwa watoto kwenye banda la NHIF.

Na Editha Karlo | Geita | MKUU wa Mkoa wa Geita Enjinia Robert Gabriel ameupongeza mfuko wa bima ya afya (NHIF) kwakuweka utaratibu mzuri wa kutaka kila mwananchi awe na kadi ya bima ya afya.

Mkuu wa Wilaya ya Geita Fadhil Juma ameyasema hayo leo kwenye banda la mfuko wa bima ya afya (NHIF) akimwakilisha Mkuu wa Mkoa huo kukabidhi kadi za bima ya afya kwa watoto wenye umri chini ya miaka 18 mpango unaoitwa toto afya.

Hafla hiyo ya makabidhiano ya kadi hizo kwa watoto imefanyika kwenye banda la NHIF kwenye viwanja vya Maonesho ya tatu ya Kimataifa ya Teknolojia na Uwekezaji kwenye Sekta ya Madini yanayoendelea Mjini Geita Mkuu huyo wa Mkoa amewahimiza Watanzania kuchangamkia fursa ya kuwa na bima ya afya kwa kuwa milango imefunguliwa kwa kila Mwananchi.

"Nina waomba wananchi kuchangamkia hii fursa ya kila mmoja kuwa na bima ya afya kwakuwa sasa tayari milango ipo wazi kama mnavyoona serikali yetu imeboresha sana katika sekta ya afya" alisema.

Meneja wa NHIF Mkoani Geita Elius Odhiambo amesema NHIF inampango wa bima  ya afya kwa kila  mtu huku  akiyataja hayo  makundi yanayosajiliwa kuwa ni Watumishi,Watoto wenye umri chini ya miaka 18, wanafunzi, wakulima, wamachinga na watu binafsi.
Makundi mengine ni wachimbaji wadogo wa madini, madereva, Waendesha boda boda na wajasiriamali katika vikundi mbalimbali  vya kiuchumi.

Odhiambo alisema viwango vya kujiunga vinatofautina kutokana na kundi ila kadi za toto afya kadi za watoto wenye umri chini ya miaka kumi na nane ni shilingi 50,400 kwa mtoto kwa mwaka.

"Siku zote ugonjwa huwa unakuja bila ya taarifa,kuna siku unaweza kuugua huna pesa ya matibabu lakini kama una kadi yako wa bima ya afya utakuwa na uhakika wa matibabu wewe na familia yako hata kama umeugua huna pesa" alisema Odhiambo.

No comments:

Post a Comment

Absa Dar City Marathon 2024 donates hospital equipment to Mnazi Mmoja Hospital

Absa Bank Tanzania Head of Marketing and Corporate Affairs, Mr. Aron Luhanga hands over a part of hospital equipment to Mnazi Mmoja Hospital...

Pages