Marekani yataka Armenia na Azerbaijan kukumbatia Diplomasia - THINKING IN BUSINESS

Mgongopr.blogspot.com is a business centered online platform highlighting trade, finance and economic news in Tanzania. Our coverage is customised to ensure we consolidate brands, boost sales and nurture investments. The site is an imprint of Mgongo Logistics and Solutions, a trusted consultancy firm, offering Social Media Management, Photography, Videography, Advertising, Event Management and Translation. For more information contact us via; Phone: +255 767765454, email: mgongo@gmail.com

Breaking

Wednesday, October 28, 2020

Marekani yataka Armenia na Azerbaijan kukumbatia Diplomasia


Na Patrick Nduwimana | Washington DC | Waziri wa mambo ya nje wa marekani Mike Pompeo amezisihi Armenia na Azerbaijan kufikia suluhisho la kidiplomasiya kuhusu mzozo kati yao wa kudhibiti jimbo lenye ugomvi la Nagorno Karabakh, ambako ghasia zilizoanza miezi miwili iliopita ziliendelea jana jumanne, licha ya mkataba wa kusitisha mapigano uliofikiwa na pande zote mjini Washington.

Akiwa ziarani nchini India, Pompeo alizungumza kwa njia ya simu na waziri mkuu wa Armenia Nikol Pashinyan pamoja na rais wa Azerbaijan Ilham Aliyev.

Pompeo amewashinikiza viongozi hao wawili kutekeleza ahadi zao za kusitisha mapambano na kutafuta suluhisho la kidiplomasiya, taarifa ya wizara ya mambo ya nje ya marekani imesema.

Jumanne, nchi mbili kila mmoja imeishtumu nyingine kushambulia ngome zilizoko nje ya Nagorno Karabakh, baada ya mkataba wa sitisho la mapigano uliopatikana kutokana na juhudi za waziri Pompeo.

No comments:

Post a Comment

SERIKALI YASISITIZA UTAALAMU NA UBUNIFU KATIKA UNUNUZI NA UGAVI

Serikali imewataka wataalam wa ununuzi na ugavi nchini kuongeza ubunifu, uongozi bora na matumizi ya teknolojia za kisasa ili kuongeza ufani...

Pages