Benki ya Absa yatoa msaada wa vifaa vya usafi kwa shule za Dodoma - THINKING IN BUSINESS

Mgongopr.blogspot.com is a business centered online platform highlighting trade, finance and economic news in Tanzania. Our coverage is customised to ensure we consolidate brands, boost sales and nurture investments. The site is an imprint of Mgongo Logistics and Solutions, a trusted consultancy firm, offering Social Media Management, Photography, Videography, Advertising, Event Management and Translation. For more information contact us via; Phone: +255 767765454, email: mgongo@gmail.com

Breaking

Monday, February 1, 2021

Benki ya Absa yatoa msaada wa vifaa vya usafi kwa shule za Dodoma

Mwakilishi wa Benki ya Absa tawi la Dodoma, Elizabeth Kiwale (wa pili kushoto), akimkabidhi vifaa vya usafi ndoo na sabuni Mwalimu  Mkuu wa Shule ya Msingi Ipagala B, Plaxeda Fundisha, ( wa tatu kulia) katika hafla ya uzinduzi wa ugawaji vifaa vya usafi kwa shule za msingi 54 ulioratibiwa na Shirika la Pact Tanzania kupitia mradi wa WASH unaodhaminiwa na Absa. Uzinduzi huo ulifanyika jana shuleni hapo, jijiji Dodoma. Wa tatu kushoto ni mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa, Mazengo Eliasi na kushoto ni Beatrice Kamugisha kutoka Pact Tanzania.

Mwakilishi  wa Benki ya Absa Tanzania, Elizabeth Kiwale akizungumza na walimu, wanafunzi, na wadau mbalimbali katika hafla ya uzinduzi wa ugawaji vifaa vya usafi kwa shule za msingi 54 vilivyotolewa kwa udhamini wa Absa, jana katika Shule Msingi Ipagala B jijini Dodoma
Wawakilishi kutoka benki ya Absa Tanzania,  Elizabeth Kiwale na Happy Alipipi pamoja na wahudhuriaji wengine wakinawa mikono kwa kutumia vifaa vilivyotolewa msaada na benki hiyo katika hafla ya ugawaji wa vifaa hivyo  kwa Shule ya Msingi Ipagala B, jijini Dodoma.
Mwanafunzi wa Shule ya Ipagala B, Jesca Saimon pamoja na mwenzake wakinawa mikono baada kukabidhiwa  vifaa vya usafi kutoka Benki ya Absa shuleni kwao, Dodoma jana.

No comments:

Post a Comment

Portwest Deepens East African Footprint with Apparel Manufacturing Investment in TanzaniaDar es Salaam, Tanzania

The Deputy Minister for Industry and Trade, Hon. Denis Londo (center), cuts the ribbon to mark the official opening of Afriport’s occupation...

Pages