TUNATAKA KUONA TAFORI ILIYOBORESHWA - WAZIRI KAIRUKI - THINKING IN BUSINESS

Mgongopr.blogspot.com is a business centered online platform highlighting trade, finance and economic news in Tanzania. Our coverage is customised to ensure we consolidate brands, boost sales and nurture investments. The site is an imprint of Mgongo Logistics and Solutions, a trusted consultancy firm, offering Social Media Management, Photography, Videography, Advertising, Event Management and Translation. For more information contact us via; Phone: +255 767765454, email: mgongo@gmail.com

Breaking

Tuesday, July 9, 2024

TUNATAKA KUONA TAFORI ILIYOBORESHWA - WAZIRI KAIRUKI

Na Happiness Shayo - Morogoro 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) ametoa rai kwa Watumishi wa Taasisi ya Utafiti wa Misitu Tanzania (Mb) kutimiza wajibu wao kuhakikisha Taasisi hiyo inaboreka na hatimaye kuchangia katika mapato ya Taifa.

Ameyasema hayo leo katika ziara yake ya kikazi alipotembelea Taasisi hiyo kwa lengo la kuangalia utendaji kazi, kusikiliza changamoto za Watumishi na kuzupatia ufumbuzi. 
Amesema katika kufikia malengo ya Taasisi ni lazima wakawa wabunifu katika utekelezaji wa majukumu yao huku Serikali ikifanyia kazi changamoto za bajeti, vitendea kazi na upungufu wa Watumishi wote zinazowakabili.

"Fuatilieni fursa za mafunzo ili kukuza utendaji kazi wenu na mjitoe kufanya kazi kwa bidii na msikate tamaa" amesisitiza. 
Aidha amewataka Watumishi hao kujiwekea mipango mbadala ya kuiongezea Taasisi hiyo mapato kwa kuandika maandiko mbalimbali ya kuomba fedha katika Taasisi zinazotoa fedha hizo akitolea mfano wa Earth Fund na nyinginezo.

No comments:

Post a Comment

MRADI WA COOKFUND UNAOFADHILIWA NA UMOJA WA ULAYA (EU) NA KUTEKELEZWA NA UNCDF WALETA MAGEUZI YA MATUMIZI YA NISHATI KATIKA TAASISI ZA UMMA

Mshauri Mkuu wa Kiufundi wa UNCDF, Bw. Peter Malika, akizungumza wakati wa makabidhiano ya vifaa vya teknolojia ya upishi salama kwa Shule y...

Pages