Sunday, April 13, 2025

Home
BIASHARA
AKIBA COMMERCIAL BANK YAJIKITA KUTOA ELIMU YA KIFEDHA KWA WAJASILIAMALI WADOGO NA WAKATI.
AKIBA COMMERCIAL BANK YAJIKITA KUTOA ELIMU YA KIFEDHA KWA WAJASILIAMALI WADOGO NA WAKATI.
Mkurugenzi Mtendaji wa Akiba Commercial Bank Plc, Silvest Arumasi (kushoto), akiwa Kwenye kikao na wateja na wajasiriamali (SMEs) kutoka Kariakoo, katikati ya kitovu cha biashara Afrika Mashariki, ili kujadili changamoto zao na kushirikiana mawazo kuhusu masuluhisho yanayoweza kukuza biashara zao hafla hiyo imefanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam. Kulia ni Afisa Mkuu wa Biashara wa Benki ya hiyo Bi Wesi Olivia.
Mkurugenzi Mtendaji wa Akiba Commercial Bank Plc, Silvest Arumasi (katikati), akiwabkatika picha ya pamoja wateja na wajasiriamali (SMEs) kutoka Kariakoo, katikati ya kitovu cha biashara Afrika Mashariki, ili kujadili changamoto zao na kushirikiana mawazo kuhusu masuluhisho yanayoweza kukuza biashara zao
Mnamo tarehe 12/04/2025 Benki ya Akiba ilifanya kikao na wateja wake na wajasiriamali (SMEs) kutoka Kariakoo, katikati ya kitovu cha biashara Afrika Mashariki, ili kujadili changamoto zao na kushirikiana mawazo kuhusu masuluhisho yanayoweza kukuza biashara zao. Hii ni sehemu ya juhudi zetu za kuwa karibu na wateja na kutekeleza dhamira yetu ya kuwawezesha wajasiriamali na kuimarisha elimu ya fedha, alisema Bi. Dora Saria Mkuu wa Kitengo cha masoko na Mawasiliano wa Benki hiyo.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo Bwana Silvest Arumasi, alielezea furaha yake kwa kushirikiana moja kwa moja na wateja, akisema, "katika Benki yetu , tunaamini kwamba mafanikio ya wateja wetu ni mafanikio yetu. Tunajivunia sana kushirikiana na wajasiriamali wote nchini katika kusaidia kukuza biashara zao kupitia elimu ya fedha, mikopo, na huduma za kidijitali."
Akizungumza katika tukio hilo, Bi. Wezi Olivia Mwazani, Afisa Mkuu wa Biashara wa Benki ya Akiba, alisisitiza umuhimu wa kujenga uhusiano ya kudumu na wateja kwa kutoa huduma za kifedha zinazolingana na mahitaji yao.
"Tunafurahi kuwa na fursa ya kuzungumza na wateja wetu moja kwa moja, kuelewa changamoto zao na kutoa masuluhisho ya kifedha ambayo yatasaidia katika mafanikio yao ya muda mrefu."
Wateja waliokuwepo waliotoa shukrani zao kwa juhudi hizo, wakielezea jinsi fursa ya kushirikiana na Benki hiyo ilivyo muhimu kwa ukuaji wa biashara zao. Wengi walielezea kuwa mpango huu wa elimu ya fedha na huduma za kidijitali utawawezesha kufanya biashara zao kwa ufanisi zaidi.
Bw. Silvest Arumasi, Mkurugenzi Mtendaji wa ACB aliwashukuru wateja kwa uaminifu wao na ushirikiano wa muda mrefu, akiongeza, "Tunapenda kuwashukuru wateja wetu wa Kariakoo na maeneo mengine kwa ushirikiano wao ikiwa ni pamoja na kutuchagua na kutuamini. Pamoja, tutaendelea kuleta mabadiliko katika sekta ya SMEs na kusaidia katika maendeleo endelevu ya kiuchumi."
Benki ya Akiba inaendelea kutoa huduma za kibenki zinazolenga mahitaji ya wateja na kusaidia ukuaji wa biashara za watu binafsi, SMEs pamoja na makampuni makubwa na taasisi mbalimbali kupitia huduma zinazokidhi mahitaji yao na matumizi ya teknolojia ya kidijitali.
Tags
# BIASHARA
Share This
Newer Article
WATU 12,000 WAHOFIWA KUUGUA UGONJWA WA HIMOFILIA NCHINI
Older Article
WADAU ZAIDI YA 500 KUSHIRIKI WIKI YA AZAKI 2025 MWEZI JULAI ARUSHA
AKIBA COMMERCIAL BANK YAJIKITA KUTOA ELIMU YA KIFEDHA KWA WAJASILIAMALI WADOGO NA WAKATI.
kilole mzeeApr 13, 2025AKIBA COMMERCIAL BANK YAPELEKA TABASAMU KWA WATOTO WANAOLELEWA CHAKUWAMA.
Hassani MakeroMar 28, 2025SIMTANK TANZANIA YATOA ZAWADI KWA MAWAKALA WAKE WAKISHEREHEKEA MIAKA 35 TANGU KUANZISHA
kilole mzeeMar 02, 2025
Labels:
BIASHARA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Mkurugenzi Mtendaji wa Akiba Commercial Bank Plc, Silvest Arumasi (kushoto), akiwa Kwenye kikao na wateja na wajasiriamali (SMEs) kutoka Kariakoo, katikati ya kitovu cha biashara Afrika Mashariki, ili kujadili changamoto zao na kushirikiana mawazo ...
No comments:
Post a Comment