Mshindi wa kampeni ya malengo ya Benki ya NBC akabidhiwa gari lake - Serious Business

Mgongopr.blogspot.com is a serious online platform of business and finance news from around Tanzania. We are a trusted site covering the entire spectrum, from small enterprises to large businesses entities. For photography, videography, media management, events management, advertising, public relations, translation, interpreters, and more services, please contact us: MPP Ltd phone: +255 767765454, email: mgongo@gmail.com

Breaking

Friday, June 3, 2016

Mshindi wa kampeni ya malengo ya Benki ya NBC akabidhiwa gari lake

Mshindi wa Kampeni ya akaunti ya Malengo ya Benki ya NBC, Erastus Mtui (wa pili kushoto), mkazi wa Jiji la Dar es Salaam akipokea ufunguo wa gari jipya aina ya Toyota Prado lenye thamani ya Dola za Kimarekani 100,000 kutoka kwa Ofisa Mwendeshaji Mkuu wa Benki ya NBC Tanzania, James Kinyany (wa pili kulia) alilojishindia katika kampeni  hiyo illiyochukua muda wa miezi mitatu. Hafla ya makabidhiano ilifanyika jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mkuu wa Huduma Rejareja za Kibenki wa benki hiyo, Mussa Jallow na kushoto ni mke wa Erastus, Violeth Mtui na watoto wao.
Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya NBC Tanzania, Neema Rose Singo akifanya mahojiano na waandishi wa habari katika hafla hiyo.​ Alisema kampeni hiyo iliyodumu kwa miezi mitatu ilikuwa na lengo la kuhamasisha wateja wao kuwa na moyo wa kujiwekea akiba kufanikisha malengo yao.
Mshindi wa Kampeni ya Akaunti Malengo ya Benki ya NBC, Erastus Mtui (katikati) akipiga picha ya kumbukumbu pamoja na familia yake ndani ya gari lao mara baada ya kukabidhiwa. Kushoto ni mkewe, Violeth na watoto wao.
Mtoto wa mshindi huyo, Praise Erastus Mtui (katikati), akielezea furaha yake baada ya baba yake kushinda zawadi ya gari.Pamoja naye ni wadogo zake.
Mshindi wa Kampeni ya Malengo ya Benki ya NBC, Erastus Mtui (kulia), akipozi kwa picha pamoja familia yake karibu na gari lao muda mfupi baada ya kukabidhiwa. Bwana Erasus mkazi wa Makongo jijini Dar es Salaam amewaomba wateja wa benki hiyo kuendelea kutumia akaunti ya Malengo ya Benki ya NBC ili kunufaika na faida mbalimbali zinazopatikana kupitia akaunti hiyo.
Maofisa wa Benki ya NBC wakiwa katika picha ya pamoja na mshindi wa kampeni ya akaunti ya Malengo ya benki hiyo pamoja na familia yake.

No comments:

Post a Comment

Minister officially launches real estate giant Coldwell Banker Tanzania and Zanzibar

Zanzibar Minister for Labour, Economy, and Investment, Shariff Ali Shariff addresses guests during the launch of Coldwell Banker Tanzania an...

Pages