Mshindi wa kampeni ya malengo ya Benki ya NBC akabidhiwa gari lake - THINKING IN BUSINESS

Mgongopr.blogspot.com is a business centered online platform highlighting trade, finance and economic news in Tanzania. Our coverage is customised to ensure we consolidate brands, boost sales and nurture investments. The site is an imprint of Mgongo Logistics and Solutions, a trusted consultancy firm, offering Social Media Management, Photography, Videography, Advertising, Event Management and Translation. For more information contact us via; Phone: +255 767765454, email: mgongo@gmail.com

Breaking

Friday, June 3, 2016

Mshindi wa kampeni ya malengo ya Benki ya NBC akabidhiwa gari lake

Mshindi wa Kampeni ya akaunti ya Malengo ya Benki ya NBC, Erastus Mtui (wa pili kushoto), mkazi wa Jiji la Dar es Salaam akipokea ufunguo wa gari jipya aina ya Toyota Prado lenye thamani ya Dola za Kimarekani 100,000 kutoka kwa Ofisa Mwendeshaji Mkuu wa Benki ya NBC Tanzania, James Kinyany (wa pili kulia) alilojishindia katika kampeni  hiyo illiyochukua muda wa miezi mitatu. Hafla ya makabidhiano ilifanyika jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mkuu wa Huduma Rejareja za Kibenki wa benki hiyo, Mussa Jallow na kushoto ni mke wa Erastus, Violeth Mtui na watoto wao.
Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya NBC Tanzania, Neema Rose Singo akifanya mahojiano na waandishi wa habari katika hafla hiyo.​ Alisema kampeni hiyo iliyodumu kwa miezi mitatu ilikuwa na lengo la kuhamasisha wateja wao kuwa na moyo wa kujiwekea akiba kufanikisha malengo yao.
Mshindi wa Kampeni ya Akaunti Malengo ya Benki ya NBC, Erastus Mtui (katikati) akipiga picha ya kumbukumbu pamoja na familia yake ndani ya gari lao mara baada ya kukabidhiwa. Kushoto ni mkewe, Violeth na watoto wao.
Mtoto wa mshindi huyo, Praise Erastus Mtui (katikati), akielezea furaha yake baada ya baba yake kushinda zawadi ya gari.Pamoja naye ni wadogo zake.
Mshindi wa Kampeni ya Malengo ya Benki ya NBC, Erastus Mtui (kulia), akipozi kwa picha pamoja familia yake karibu na gari lao muda mfupi baada ya kukabidhiwa. Bwana Erasus mkazi wa Makongo jijini Dar es Salaam amewaomba wateja wa benki hiyo kuendelea kutumia akaunti ya Malengo ya Benki ya NBC ili kunufaika na faida mbalimbali zinazopatikana kupitia akaunti hiyo.
Maofisa wa Benki ya NBC wakiwa katika picha ya pamoja na mshindi wa kampeni ya akaunti ya Malengo ya benki hiyo pamoja na familia yake.

No comments:

Post a Comment

SERIKALI YASISITIZA UTAALAMU NA UBUNIFU KATIKA UNUNUZI NA UGAVI

Serikali imewataka wataalam wa ununuzi na ugavi nchini kuongeza ubunifu, uongozi bora na matumizi ya teknolojia za kisasa ili kuongeza ufani...

Pages