Mahafali ya Sekondari ya Sullivan Provost, Kibaha kwa Mathias yafana - Serious Business

Mgongopr.blogspot.com is a serious online platform of business and finance news from around Tanzania. We are a trusted site covering the entire spectrum, from small enterprises to large businesses entities. For photography, videography, media management, events management, advertising, public relations, translation, interpreters, and more services, please contact us: MPP Ltd phone: +255 767765454, email: mgongo@gmail.com

Breaking

Friday, October 14, 2016

Mahafali ya Sekondari ya Sullivan Provost, Kibaha kwa Mathias yafana

Mkurugenzi Mtendaji wa Shule ya Wavulana ya Sullivan Provost,  Rachel Mwalukasa (kushoto), akizungumza wakati wa  mahafali ya pili ya kidato cha nne ya shule hiyo shuleni hapo, Kibaha kwa Mathias mkoani  Pwani hivi karibuni. Wengine kutoka  kulia ni Mkuu wa Shule, Alex Nicholaus, Mhadhiri kutoka  Chuo Kikuu cha Dar es Salaam,  Dk Ellen Kalinga na Mhandisi wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano ya UDSM (COICT), Dk Suzan Lujara aliyekuwa mgeni rasmi katika mahafali hayo
Mhadhiri kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk Ellen Kalinga,  (wa pili kulia) akimpongeza Mohamed Ibrahim, mmoja wa wanafunzi waliofanya vizuri kimasomo na kujizolea tuzo mbalimbali wakati wa mahafali ya pili ya kidato cha nne ya shule hiyo shuleni hapo, Kibaha kwa Mathias, Pwani hivi karibuni. Wengine kutoka Kulia ni Mhandisi wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano ya UDSM (COICT), Dk Suzan Lujara, Mkurugenzi Mtendaji wa Sullivan Provost, Rachel Mwalukasa na Mkuu wa shule hiyo, Alex Nicholaus. 
Mhandisi wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (COICT), Dk Suzan Lujara (wa pili kulia) akikabidhi cheti kwa Alvin Mgaya, mmoja wa wahitimu wa kidato cha nne wa Shule ya Sekondari ya wavulana ya Sullivan Provost wakati wa mahafali ya pili ya shule hiyo, shuleni hapo  Kibaha kwa Mathias, Pwani hivi karibuni. Wa pili kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa shule hiyo, Rachel Mwalukasa na Mhadhiri kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Dk. Ellen Kalinga
Mkurugenzi Mtendaji wa Shule ya Sekondari ya Wavulana ya Sullivan Provost,  Rachel Mwalukasa (katikati), akimlisha keki mmoja wa wahitimu wa kidato cha nne wa shule hiyo wakati wa mahafali yao ya pili shuleni hapo, Kibaha kwa Mathias, Pwani hivi karibuni.
Wahitimu wa kidato cha nne wa Shule ya Sekondari ya Wavulana ya Sullivan Provost wakipozi kwa picha ya kumbukumbu pamoja nja baadhi ya walimu, viongozi wa shule na mgeni rasmi wakati wa  mahafali yao shuleni hapo, Kihaba, Pwani.
Mkurugenzi Mtendaji wa Shule ya Wavulana ya Sullivan Provost,  Rachel Mwalukasa (katikati), akimpongeza Mkuu wa shule hiyo Alex Nicholaus  katika mahafali ya pili ya kidato cha nne ya shule hiyo shuleni hapo, Kibaha kwa Mathias, Pwani hivi karibuni. Anayeangalia ni mmoja wa wajumbe wa kamati ya wazazi wa shule hiyo, Janeth Alexander. (Picha na Brian Peter Mgongo)

No comments:

Post a Comment

Minister officially launches real estate giant Coldwell Banker Tanzania and Zanzibar

Zanzibar Minister for Labour, Economy, and Investment, Shariff Ali Shariff addresses guests during the launch of Coldwell Banker Tanzania an...

Pages