WAHARIRI WAPEWA SOMO KUHUSU UZALISHAJI SARUJI NA UBORA WAKE - THINKING IN BUSINESS

Mgongopr.blogspot.com is a business centered online platform highlighting trade, finance and economic news in Tanzania. Our coverage is customised to ensure we consolidate brands, boost sales and nurture investments. The site is an imprint of Mgongo Logistics and Solutions, a trusted consultancy firm, offering Social Media Management, Photography, Videography, Advertising, Event Management and Translation. For more information contact us via; Phone: +255 767765454, email: mgongo@gmail.com

Breaking

Monday, August 14, 2017

WAHARIRI WAPEWA SOMO KUHUSU UZALISHAJI SARUJI NA UBORA WAKE

Meneja Mawasiliano na Mahusiano ya Nje wa Kampuni ya Saruji Tanga (TCPLC), Bi. Mtanga Noor  (kulia), akiwapokea baadhi ya wahariri wa habari wakati wa ziara ya wahariri wa habari za biashara na uchumi  kutoka vyombo mbalimbali vya habari walipotembelea kiwanda cha kampuni hiyo, Pongwe, Tanga juzi kujionea shughuli mbalimbali za uzalishaji saruji, mipango ya maendeleo na changamoto zinazowakabili.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Saruji Tanga (TCPLC), Reinhardt Swart (kulia, akizungumza wakati wa  ziara ya wahariri hao walipotembelea kiwandani hapo, Pongwe, Tanga juzi kujionea shughuli za uzalishaji wa saruji na mipango ya maendeleo ya kampuni hiyo.

Mmoja ya waandishi wa habari mkoani Tanga, Mngazija akijitambulisha wakati wa ziara hiyo.

Baadhi ya maofisa na wataalamu wa Kampuni ya Saruji Tanga wakiwa tayari kutoa elimu kuhusu uzalishaji saruji na kujibu maswali wakati wa ziara hiyo.

Meneja Usambazaji  wa TCPLC, Samuel Shoo (kulia),  akitoa elimu kuhusu hatua mbalimbali za uzalishaji  saruji na ubora wake kwa wahariri hao.

Baadhi ya wahariri wa habari za biashara na uchumi wakiwa katika chumba cha kuendeshea mitambo cha kampuni hiyo.

Meneja Machimbo wa Kampuni ya Saruji Tanga (TCPLC), Godwin Kamando (kulia), akitoa maelezo kuhusu shughuli za uchimbaji mawe katika eneo la machimbo ya kampuni hiyo wakati wahariri wa habari za biashara na uchumi kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini walipotembelea kiwanda cha kampuni hiyo, Pongwe, Tanga juzi kujionea shughuli za uzalishaji wa saruji.

No comments:

Post a Comment

ABSA BANK TANZANIA REAFFIRMS COMMITMENT TO SUPPORTING TANZANIA’S HEALTH SECTOR

Absa Bank Tanzania Managing Director, Obedi Laiser (right), competes alongside other participants during the 10-kilometre race of the 2026 A...

Pages