RC MAKONDA AONGEZA MUDA WA KUSIKILIZA MALALAMIKO YA WANANCHI WAKE - THINKING IN BUSINESS

Mgongopr.blogspot.com is a business centered online platform highlighting trade, finance and economic news in Tanzania. Our coverage is customised to ensure we consolidate brands, boost sales and nurture investments. The site is an imprint of Mgongo Logistics and Solutions, a trusted consultancy firm, offering Social Media Management, Photography, Videography, Advertising, Event Management and Translation. For more information contact us via; Phone: +255 767765454, email: mgongo@gmail.com

Breaking

Friday, February 2, 2018

RC MAKONDA AONGEZA MUDA WA KUSIKILIZA MALALAMIKO YA WANANCHI WAKE

Kutokana na idadi kubwa ya Wananchi waliojitokeza kupata msaada wa kisheria Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda ameamua kuongeza siku moja hadi kesho ili kuhakikisha wananchi wote waliofika wanasikilizwa na kuhudumiwa.
Akiongea kwa niaba ya RC Makonda, Mwenasheria wa ofisi ya mkoa wa Dar es salaam Fabiola Mwingira amesema idadi ya wananchi waliojitokeza ni kubwa* tofauti na matarajio lakini wamejitaida hadi sasa zaidi ya Wananchi 3,000 wamepatiwa huduma.

RC Makonda pia amewatangazia Wananchi wote waliosikilizwa na wanasheria kufika ukumbi wa Diamond Jubilee ifikapo Tarehe 10 February kuanzia Saa moja Asubuhi kwaajili ya kupatiwa mrejesho.

Taarifa za kuongezwa kwa muda zimepokelewa kwa shangwe na Wananchi ambapo wamemsifu RC Makonda kwa kutanguliza Utu mbele kwa kuhakikisha wanyonge wanaipata haki yao waliyotaabika kuitafuta kwa miaka mingi.

HONGERA RC MAKONDA KWA KUTIMIZA NDOTO YA RAIS MAGUFULI.

No comments:

Post a Comment

APeF Yazindua Mfuko wa Ziada Kupanua wigo wa uwekaji Akiba, Uwekezaji na Ulinzi

  Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana, (CMSA), CPA Nicodemus Mkama, akikabidhi waraka wa ofa kwa Kaimu Mwenyekiti ...

Pages