MBUNGE SOPHIA MWAKAGENDA ATWAA TUZO YA DUNIA - THINKING IN BUSINESS

Mgongopr.blogspot.com is a business centered online platform highlighting trade, finance and economic news in Tanzania. Our coverage is customised to ensure we consolidate brands, boost sales and nurture investments. The site is an imprint of Mgongo Logistics and Solutions, a trusted consultancy firm, offering Social Media Management, Photography, Videography, Advertising, Event Management and Translation. For more information contact us via; Phone: +255 767765454, email: mgongo@gmail.com

Breaking

Sunday, March 24, 2019

MBUNGE SOPHIA MWAKAGENDA ATWAA TUZO YA DUNIA


Mhe. Sophia Hebron Mwakagenda - Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Mbeya (CHADEMA) ambaye pia ni Mwanaharakati wa siku nyingi wa Wanawake na Watoto amepewa tuzo ya heshima ya "A Woman of the decade in Public life" iliyotolewa katika Mkutano maalumu wa Woman Economic Forum unaofanyika New Delh India ulioanza tarehe 26 April na utamalizika tarehe 01 May 2018 na unaoshirikisha Wanawake zaidi ya 2000 kutoka pande mbalimbali za dunia wakiwemo Viongozi na wale walioonyesha mabadiliko chanya katika jamii.


Katika mkutano huo Mhe. Sophia pia alipata fursa ya kuongea na Wanawake hao kutoka pande zote za dunia na pia amekuwa mwanamke pekee kwa Afrika Mashariki kukabidhiwa tuzo hiyo ambayo ni ya heshima kutokana na mchango wake mkubwa wa muda mrefu katika kusaidia wanawake na watoto nchini Tanzania ikiwemo kielimu, kiafya na kiuchumi ikiwemo juhudi zake anazofanya katika kuwawezesha wanawake katika msaada wa kisheria na katika kuwapa mafunzo ya ujasiriamali na kuwasaidia vifaa vya kufanyia shughuli zao ikiwemo vyerehani na vifaa vingine.

Habari katika Picha na Anna Peter

No comments:

Post a Comment

SERIKALI YASISITIZA UTAALAMU NA UBUNIFU KATIKA UNUNUZI NA UGAVI

Serikali imewataka wataalam wa ununuzi na ugavi nchini kuongeza ubunifu, uongozi bora na matumizi ya teknolojia za kisasa ili kuongeza ufani...

Pages