Benki ya NBC Kitengo cha Retail chawazawadia wafanyakazi wake bora - Serious Business

Mgongopr.blogspot.com is a serious online platform of business and finance news from around Tanzania. We are a trusted site covering the entire spectrum, from small enterprises to large businesses entities. For photography, videography, media management, events management, advertising, public relations, translation, interpreters, and more services, please contact us: MPP Ltd phone: +255 767765454, email: mgongo@gmail.com

Breaking

Tuesday, February 2, 2016

Benki ya NBC Kitengo cha Retail chawazawadia wafanyakazi wake bora

Mkuu wa Mtandao wa Wateja wa NBC Bw. Gaudence Shawa akimkabidhi cheti Bw. Nelson Moshi kwa kuwa mmoja wa wauzaji bora wa NBC kwa mwaka 2015 wakati wa hafla ya Retail Council Awards, iliyofanyika jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Wafanyakazi wa NBC idara ya huduma reja reja za kibenki wakisherekea na mwenzao, Evance Luhimbo (Mwenye vazi la Kimasai) kwa kuibuka Meneja Kanda bora wa Mwaka 2015 wakati wa hafla ya Retail Council Awards, iliyofanyika jijini Dar es Salaam. Wengine kwenye picha ni (waliosimama kutoka kushoto) Mkuu wa kitengo cha mikopo, Bw. Andrew Lyimo (kushoto), Mkuu wa Mauzo, Bw. Mongateko Makongoro, Mkuu wa kusimamia hatari za uendeshaji Bw. Arnold Mhally na Mkuu wa Huduma Reja Reja Za Kibenki Bw. Musa Jallow. Wengine kwa mbele ni Bw. Andrew Massawe na Bi Jaqueline Sindano.
Mkuu wa Mtandao wa Wateja wa NBC Bw. Gaudence Shawa akimkabidhi cheti Bw. Methody Tryphone (kulia), kwa kuwa mmoja wa wauzaji bora wa NBC kwa mwaka 2015 wakati wa hafla ya Retail Council Awards, iliyofanyika jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Kushoto ni Meneja Uendelezaji wa Biashara wa NBC Bw. Eddie Mhina.
Meneja Tawi la NBC Sea Cliff Bi. Mariam Kombo (Kulia) akipokea tuzo ya Meneja Tawi Bora kutoka kwa Mkuu wa Idara ya Uzingatiaji na Utekelezaji wa sheria za Fedha (compliance and regulatory affairs) wa NBC, Bi.Sarah Laiser-Sumaye, kwenye hafla ya Retail Council Awards, iliyofanyika jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Kaimu Mkuu wa Huduma za Digitali na njia za huduma mbadala, wa NBC, Bi. Cynthia Ponera (wa pili kushoto), akipokea Tuzo ya Mkuu wa Huduma Reja Reja za Kibenki kutoka kwa Mkuu wa Idara hiyo Bw. Musa Jallow wakati wa hafla ya Retail Council Awards, iliyofanyika jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Wengine kwenye picha ni Mkuu wa kitengo cha mikopo, Bw. Andrew Lyimo (kushoto), Mkuu wa Mauzo, Bw. Mongateko Makongoro, Mkuu wa Huduma za Kibenki Binafsi, Bi. Ashura Waziri, na Mkuu wa Usimamizi wa Taarifa, Bi.Tulibako Paiti.
Mkuu wa Idara ya Huduma Reja Reja za Kibenki Bw. Musa Jallow, akimvisha Bw.Robert Kimaro vazi la kimasaai baada kutangazwa kuwa miongoni mwa wauzaji Bora wa mwaka 2015 wakati wa hafla ya Retail Council Awards, iliyofanyika jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Wengine kwenye picha ni Meneja Uendelezaji wa Biashara wa NBC Bw. Eddie Mhina na (kushoto) na Mkuu wa Mauzo wa NBC Bw. Mongateko Makongoro.

No comments:

Post a Comment

Absa Dar City Marathon 2024 zatimua vumbi jijini Dar es Salaam

Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Absa Tanzania, Bwana Aron Luhanga (kushoto), akikabidhi zawadi kwa mshindi wa kwanza wa mbio za nu...

Pages