BENKI YA NBC YATOA SHILINGI BILLION 2.1 KUKOPESHA WASTAAFU - THINKING IN BUSINESS

Mgongopr.blogspot.com is a business centered online platform highlighting trade, finance and economic news in Tanzania. Our coverage is customised to ensure we consolidate brands, boost sales and nurture investments. The site is an imprint of Mgongo Logistics and Solutions, a trusted consultancy firm, offering Social Media Management, Photography, Videography, Advertising, Event Management and Translation. For more information contact us via; Phone: +255 767765454, email: mgongo@gmail.com

Breaking

Friday, July 19, 2019

BENKI YA NBC YATOA SHILINGI BILLION 2.1 KUKOPESHA WASTAAFU

9Y4A7670
Meneja wa Kanda ya Mashariki wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Venance Mashiba (wa pili kulia), na Mkurugenzi Wateja Binafsi wa Benki ya NBC, Gaudence Shawa (kulia kwake), wakikata keki kusherehekea uzinduzi rasmi tawi jipya la Benki ya NBC Tegeta katika jengo la Kibo Complex, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam hivi karibuni. Wengine kutoka kushoto ni, Mkurugenzi wa Kitengo cha Makampuni, Linley Kapya, Mnadhimu Mkuu Ofisi ya Mkurugenzi Mkuu wa benki hiyo, Joyce Mbago, Meneja wa Tawi la Tegeta, Edward Chibombo na Mkurugenzi wa Fedha, Waziri Barnabas.
9Y4A7655
Meneja wa Kanda ya Mashariki wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Venance Mashiba ( wa nne kushoto), na Mkurugenzi wa Wateja Binafsi wa Benki ya NBC, Gaudence Shawa (kushoto kwake), wakikata utepe kuzindua rasmi tawi jipya la Benki ya NBC Tegeta nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam. Wengine kutoka kushoto ni, Mkurugenzi wa Kitengo cha Makampuni, Linley Kapya, Mnadhimu Mkuu Ofisi ya Mkurugenzi Mkuu wa benki hiyo, Joyce Mbago, Mkurugenzi wa Fedha, Waziri Barnabas na Meneja wa Tawi la Tegeta, Edward Chibombo.
9Y4A7575
Kaimu Mkurugenzi wa Wateja Binafsi wa Benki ya NBC, Gaudence Shawa, akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa Tawi jipya la benki hiyo la Tegeta katika jengo la Kibo Complex jijini Dar es Salaam.
9Y4A7738
Kaimu Mkurugenzi wa Wateja Binafsi wa NBC, Gaudence Shawa (katikati waliokaa) Mkurugenzi wa Kitengo cha Makampuni, Linley Kapya (kulia kwake) na Mkurugenzi wa Fedha, Waziri Barnabas (kushoto kwake), wakiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi katika tawi hilo na baadhi ya maofisa wa NBC katika hafla hiyo.
Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) nchini imetoa mikopo yenye jumla ya kiasi cha shilingi Billioni 2.1 kwa wastaafu tokea ilipozindua huduma ya mikopo ya wastaafu Juni mwaka jana.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Theobald Sabi, Mkurugenzi wa Wateja Binafsi, Bw Gaudence Shawa katika hafla ya uzinduzi rasmi wa Tawi jipya la Benki hiyo la Tegeta Kibo Commercial Complex alisema kwamba benki hiyo imewatambua wastaafu kama kundi muhimu la kiuchumi.

“NBC tumewatambua wastaafu wanaopokea pensheni kama kundi la kiuchumi ambalo lina uwezo wa kuchangia katika uchumi wa taifa letu kwa kuwezeshwa kifedha,” 

No comments:

Post a Comment

Absa Bank Tanzania Celebrates Record-Breaking Success at the 2026 Tanzania Pickleball Open, Reinforcing Nation’s Vision as a Regional Sports Hub

  Absa Bank Tanzania Celebrates Record-Breaking Success at the 2026 Tanzania Pickleball Open, Reinforcing Nation’s Vision as a Regional Spor...

Pages